MWENYEKITI WA UMOJA WA VIJANA WA CCM TAIFA NDUGU KHERI JEMES AKIZUNGUMZA NA WAAANDISHI WA HABARI AKITOA TAMKO LA KUELEKEA KILELE CHA MATEMBEZI YA MIAKA 56 YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR YALIYOJUMUISHA ZAIDI YA VIJANA 500 KUTOKA MIKOA YOTE YA TANZANIA BARA NA ZANZIBAR.
katika kikao hicho amewasihi vijana kuendelea kunga mkono kwa nguvu zote kwani mapinduzi hayo yamesaidia kuwakomboa wanyonge na kuwaomba vijana hao kuachana na maneno ya kejeli yanayotolewa na wasiotakia mema nchi yetu .
Pia Katika kikao hicho aliwaasa vijana kuendele a kuyaenzi mapinduzi matukufu kwani yalikuwa na malengo makuu matatu ambayo ni kuenzi historia ya mapinduzi, utatashi wa kujiongoza wenyewe, kuwa na kihakikisha rasili mali zilizokuwepo Zanzibar zinabaki kuwa ni rasili mali za wazanzibari wenyewe.
pia ameendelea kusema kwamba kwa kuyaenzi mapinduzi umoja wa vijana hautakubali wala kuwafumbia macho wale ambao wanayabeza mapinduzi hayo kwa faida zao na atahakikisha watambambana nao kwa namna yoyote ile kwani mapinduzi hayo yana faida kwa wananchi na yamesaidia katika kukuza miradi mbali mbali ya kimaendeleo.
#Viva vijana viva
#MAPINDUZI_DAIMA
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni