Jumapili, 12 Januari 2020

#BARIADI :- DC BARIADI AMTEMBELEA MWANAFUNZILAMECK LUGEDENGA ALIEPATA A MASOMO YAKE YOT E TISA

#BARIADI :- DC BARIADI AMTEMBELEA MWANAFUNZILAMECK  LUGEDENGA ALIEPATA A MASOMO YAKE YOT E TISA

Festo Kiswaga- DC Bariadi,Leo nimemtembelea  kijana yohana lameck lugedenga aliyefaulu mtihani wa kidato  cha nne kwa kupata  A masomo yote tisa, kutoka  shule ya igaganulwa  kata ya dutwa wilaya ya Bariadi, mkoa wa Simiyu,  . Hapa ndio nyumbani kwao. Baba yake mzazi kijana huyo alimtelekeza  akiwa darasa la tano. Inasemekana alitokomea kusikojulikana kutokana na hali ngumu ya maisha lakini zaidi kukimbia majukumu ya kulisha familia yake. Hapa Chini ni nyumbani kwa mama yake Masalu  Lulyalya . Picha ya Kwanza ni mimi na kijana huyu mwenye akili sana maana hata mtihani wa form two  alipata A nane na B moja. Picha ya pili ni mimi na mama yake mzazi. Na picha ya tatu ni mimi, mama  yake pamoja na bibi yake Mbuke Limbu. Niliposikia historia ya familia hii initia hamasa sana na kumshukuru sana Mh Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa awamu ya tano Dr John Pombe Magufuli kwa kuleta elimu bure maana taarifa ni kwamba kijana huyu hata uniform za shule kwa miaka yote alikuwa ananunuliwa na walimu wake kwa vile alijulikana kwa kuwa na akili nyingi sana. Je isingekuwa elimu bure ingekuwaje kwa watoto Hawa kutoka familia masikini . AHSANTE DR JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI kwa maono  ya hali ya juu kwa waTanzania wako Hawa. Yohana amexlelewa na mama yake pekee.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni