MAMA VANESSA
SEHEMU YA 6
WHATSAPP 0655585220
ZANZIBAR
Mara simu yake iliita na alipoipokea swali lilikuwa amekaa wapi. Akamweleza na alishangaa kumuona Yule mwanamke akiongoza moja kwa moja mpaka pale alipokuwa amekaa. Lucas macho yalibaki yamemtoka na kuduwaa. Alipigwa na butwaa maaa na alaishindwa kuolewa kuw ahuyo ni mmama au mdada.
“Samahani sana kwa kuchelewa na kutopokea simu yako kwa wakati..Nikiwa naendesha gari huwa sipendi kupokea simu.
“Sawa karibu mama Vanessa” alisema Lucas huku akiendelea kumkagua hasa sehemu za kifuani. Kwa mawazo yake ya kupenda ngono tayari alishaanza kuwaza vitu ambavyo hakustahili kabisa..
“Kama nilivyojitambulisha mwanzo mimi naitwa mama Vanessa mwanamke maarufu hapa mjini na ni mke wa boss wako..
“Mke wa Boss wangu?”
“Ndio mimi ni mke wake na ndoa yetu ndo kwanza ina mwaka mmoja alinioa mimi mara baada ya mke wake wa kwanza kufariki..Nafikiri kipindi hicho wewe ulikuwa bado hujaja.
“Ni kweli hata mimi nilishasikia kuwa boss alifiwa na mke wake”.
“Kwa hiyo nimekuita hapa kwa ajili ya mpango wa kulipa kisasi. Nakuomba unisikilize kimakini sana maana tunaweza kuwa rika moja. Kwanza boss wako ana mtoto anayeitwa Vanesa mtoto huyu alikuwa mdogo wakati mama yake anafariki kwa hiyo usijefikiri mimi ni mkumbwa. La hasha mimi ni mdogo ila nimejikuta nikiingia kwenye maisha ambayo sikuyatarajia. Pesa na upendo wa uwongo umenifanya niolewe na boss wenu. Kwa sasa sina amani kabisa na sina furaha aninipa kila kitu isipokuwa mapenzi.
Hana mapenzi ya kweli amekuwa Malaya yaani anabadilisha wanawake kama nguo. Yaani huyu baba ana mtoto wake mkumbwa ambaye ndo ameingia chuo huwezi amini huyo motto na baba yake ni kitu kimoja. Mtoto anadiriki kumtafutia baba yake wanawake. Yaani anawaunganisha na rafiki zake.Nanyanyasika sana mimi na uzuri wangu huu baba Vanesa anatembea mpaka na wasichana wadogo ambao hata hawana mvuto kunizidi mimi. Ninajua kila kitu kuhusu wewe najua jinsi gani ulivyonyanyasika mpaka ikafikia kusimamishwa kazi na mbaya zaidi amemchukua mke wako. Nasikia amempa moja ya nyumba zake ambazo amejenga kwa siri ambazo hata sisi wanafamilia hatuzijui. Kwa nini huyu mwanaume anafanya hivi tena kwa vijana wadogo kama ninyi?”
Mama Vanessa aliongea kwa uchungu sana huku akifuta machozi. Alikuwa na hisia ambazo kwa kweli Lucas hakutarajia.
“Pole mama Vannesa na mimi naumia sana, naumia kuliko hata unavyoweza kufikiri, embu tazama hizi picha kisha ndo utagundua kuwa huyo mumeo sio mwanadamu kabisa, hana utu ni mnyama aliyepitiliza”
Lucas alimpa simu yake na kuanza kumuonesha picha zile ambazo alimpiga akiwa na mkewe huko Mwanza. Mwanaume huyo hakuamini na badala yake alianza kulia kwa nguvu. Alilia kama mtoto jambo lilomfanya Lucas aanze kumbembeleza…
Katika kitu ambacho Lucas huwa kinamnyima raha ni kuona mwanamke akilia mbele yake. Yaani yeye mwanamke akijilIza basi huwa anamwamini kupita kiasi. Alimbembeleza mpaka Mama Vanesa akanyamaza. Kwikwi zilimkaba sana na alikuwa akiona kabisa kijana huyo ameonewa. Mwanzo hakuwa na ushahidi wa moja kwa moja lakini zile picha zinazomuonesha mme wake akiwa na mke wa Lucas zilimuuma kupita maelezo.
“Kwa hiyo haya yote yametokea nini sasa kifanyike” Lucas alihoji mara baada ya mama huyo kubembelezwa na kurudi katika hali yake ya kawaida.
“Ndo maana nimekuita hapa ili tupange mambo na ikibidi tumkomeshe”
“Wewe unataka tumfanyeje hili hali yeye ni boss mwenye fedha. Nikikuruka na kujifanya mjuaji sana ndo nafutwa kazi kabisa.”
“Siku zote usikubali kupoteza haki yako kisa kuogopa kufukuzwa kazi. Usikubali kunyang’anywa mke au hata uhuru wako kisa pesa. Nakuambia tukiungana mimi na wewe tutafanikiwa kwa hili. Dawa ya moto ni moto na hivi tunaushahidi, hiyo kazi huwezi kufukuzwa. Mimi ndo Emmy hilo jina la mama Vanessa ni la heshima tu.
“Sawa Emmy ingawa nitapenda kukuendelea kukita mama Vanesa ni jina zuri linatamika vizuri. Ingawa mtu anavuta taswira laba ni mama kweli”.
“Kila mwanamke ni mama maana hata kama bado hajazaa ipo siku atakuja kuzaaa”. Sio mbaya ukiiita hivyo maana hata Vanesa mwenyeewe anajua kuwa mimi ndo mama yake. Alifafanua mama huyo.
“Sawa lakini bado sijajua mpango mkakati ni upi?
“Ni mdogo tu ukitendwa tenda, ukipendwa pendwa”.
Maneno hayo yalikuwa bado yanamuacha njiapanda Lucas Manyama hakujua mwanamke huyo alikuwa akitaka nini hasa kutoka kwake. Maneno hayo kwake yalikuwa yakiahshiria kuwa mama huyo alikuwa akitaka alipe kisasi kwa wao kuwa wapenzi. Kuna vitu vilikuwa vikimtatiza kwanza kwa nini mama huyo alichagua njia hiyo ya kulipa kisasi kwa nini wasipeleke ushahidi a idara ya kazi na kueleza kuwa alikuwa akisimamishwa kazi kwa sababu ya hujuma za boss wake ambaye alitumia uboss kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mkewe. Hili jambo lilimuumiza sana hasa akikumbuka ni mbali sana alipotoka. Alifikiria jinsi alivyomsomesha mke wake tena kwa tabu mpaka akafanikiwa kupata elimu na baadaye kazi. Alifikiria tukio la yeye kusimamishwa kazi na kuona kabisa haikuwa sawa. Wakati Lucas akiwaza na kuwazua mara simu ya mama Vanesaa ikaita.
Mama Vanesaa aliangalia na kusita kupokea maaana aliyekuwa akipiga ni baba Vanessa. Simu haikukukoma maana ilivyokata ikapigwa tena na safari hii mama Vanesaa alipokea.
“Upo wapi mke wangu maana ndo nimerudi kutoka Mwanza kwenye semina nimefika nyumbani sijakukuta?”
“Nimetoka kidogo mme wangu na si muda mrefu nitakuwa hapo kuna vitu tu nilienda kuvinunua kwa ajili ya safari yangu ya kesho.”
“Sawa huwai kurudi basi maana nimekumisss sana na nimekuletea zawadi nzuri mke wangu..
“Usijali honey nakuja”.
Lucas Manyama alikuwa ametega sikio na kusikiliza kila kitu kilichokua kikzungumzwa. Aliisikia vyema sauti ya boss wake. Roho ilimuuma na hakutarajia kwa picha zile zikimuonesha mke wake na boss wake wamekumbtaina wakicheza musiki Mama Vanesa angeweza toa majbu ya kukera yenye hasira. Na mama Vanesa hasingeongea hivyo kama vile hakuna kitu kibaya kilichotokea. Alitarajia mwanamke huyo atamtukana mwenyewe.
“Samahani boss wako amepiga na usiumie kwa mimi kuongea naye vizuri. Cha msingi tambua namtafutia dawa ya kumkomesha na mimi siku zote maishani mwanangu huwa sipendi kukurupuka na iktokea tatizo huwa natafuta njia ambayo itamuumiza muhusika. Kwa hiyo mkakati upo hivi mimi naenda Dar nitakaa kwa muda wa wiki moja kisha nitardi. Baada ya hapo tutakutana lakini nakuomba kwa wakati huu tuwe makini sana usikurupuke katika maumivu tufanya kama hakuna kibaya cha kuumiza moyo kilichotokea. Mama Vanesaa baada ya kusema hayo alifungua pochi yake na kutoa burungutu la pesa na kumkabidhi. Alitabasamu na kumuaga. Lucas alitamani amwambie hasiondoke lakini tayari ilikuwa ni hatari kama mme wake alishakuwa mjini. Mme wake licha ya kuwa boss katika benk ambayo alikuwa akifanya Lucas pia alikuwa ni mfanyabiashara hapo Musoma na nadiriki kusema alikuwa tajiri. Mama Vanesaa kazi yake kubwa ilikuwa kusimamania biashara hizo. Kwa hiyo ni mwanamke ambaye alikuwa akikutana na pesa karibu kila siku.
Kwa Lucas kupewa fedha ilikuwa zaidi ya ushindi kwa sababu alikuwa hana pesa kabisa. Yaani mfukoni alikuwa amebakiza shilingi elfu 10 na tayari account yake ya benk ilikuwa ikisoma ziro.Baada ya mama Vanesa kuondoka yeye alihesabu zile pesa na kukuta zilikuw laki moja. Alitabasamu na kusema asante Mungu kwa kuendelea kumsaidia kupitia watu.Aliamua kuondoka eno hilo maana anajijua kabisa akikaa baaa hachelewi kuanza kutamani kunywa pombe. Alimwita muhudu akamlipa na huyo akaeleka zake nyumbani kwake alipopangisha mitaa ya Iringo. Alifika akawasha Tv na kuendelea kuangali movie. Lengo lilikuwa ni kupoteza muda na mawazo aliyokuwa nayo. Alimwanza mama Vanesa jinsi alivyoumbika akashindwa kuelewa kwa nini boss wake hatulii wakati ana mke mzuri.
Siku ikawa imeisha hivyo na usiku mama Vanesaa alimtumia sms akimtakia usiku mwema. Usiku pia alimkumbuka Juliaana binti ambaye alimpa mapenzi usiku wa jana na kumfanya hasahu shida kwa muda. Alifikiria mengi na kujikuta akinyanyua simu na kumpigia rafiki yake Kimaro. Alikumbuka fadhila ambazo alimtendea na alimweleza kilichoendelea baada ya yeye kufika Musoma.
“Hapo mbaba ndo muda wa kulipa kisasi boss si kakupokonya mke wako na wewe fanya kweli. Tena kwa jinsi ulivyonielezea ni kwamba huyo mwanamke anataka duduuu.
Kimaro alabaki akiangua tu kicheko na kumwambia yeye anachohofia ni kushindana na watu wenye pesa maana kazi atakosa na gerzani ataingia.
“Kuhusu kazi usiogope mbaba nitakutafutia hata sehemu ya kujishikiza ila wewe kula huyo sijui mama Vanessa. Na ukifanikiwa nipigie picha mkiwa naye chumbani mimi nitajua cha kufanya. Nitalipa ghali ….aaaaaaaaaaaaaah. Hapa ni mjini hatuwezi sumbuliwa na mtu sijui kisa ana vichenji.”
Wakati wakiendelea kuongea na kupeana mbinu mbaya za kupambana na matatizo yaliyotokea simu ya Lucas ilikuwa ikiita. Alivyokata tu ikaita tena na kuangalia alikuwa Mishel mke wake wa ndoa.
Yaani alijikuta akianza kutetemeka bila yeye kupenda. Hukujua kwa nini mkewe alikuwa akimpigia wakati huo. Alishindwa kabisa kuamini kama mkewe ambaye alikuwa hapatikani takribani wiki mbili sasa ndo huyo alikuwa akimtafuta. Alisita kuipokea na aliiacha maana tayari hasira zilikuwa zimempanda kupita kiasi.Baada ya yeye kukataa kupokea simu kwa hiyari yake kuna sms iliingia.
“Kwa mjinga huenda kicheko kwa mwelevu huenda kilio.Nashukuru kwa kutopokea simu yangu. Ila tambua mimi ni mke wako wa ndoa na hakuna cha kututenganisha.”
Lucas alirudia kuisoma ile SMS na kujikuta akizidi kuchanganyikiwa maana maisha yalikuwa yakimchanganya kwa kiasi kikumbwa.Alitamani hata kulia lakini alilia machozi yaliyoishia ndani ya moyo wake. Kijasho chembamba kilimtoka na kujikuta akiwasha feni ili hewa iiingie. Bado hakupata hafueni na akaamua kutoka nje kabisa. Alikuwa kifua wazi huku akitamani hata kunywa pombe. Alikaa hapo kwenye kibaraza cha nyumba. Mawazo ya uchngu yalizidi kuunyanyasa ubongo wake. Moyo wake ulizidi kunyong’onyea kwa hasira ya mambo ambayo yalikuwa yakiendelea. Alitamani ardhi ifunguke na yeye aingie ndani. Maisha kwake yalikuwa ni mtihani mkumbwa sana ambao kwa kweli uliitaji nguvu za ziada kukabialiana nao. Nyumba aliyokuwa akiishi ni nyumba ambayo ilikuwa ikiongozana na Lodge. Kwa hiyo wakati akiwaza na kuwazua macho yake aliyaelekeza moja kwa moja kwenye lodge hiyo. Aliona gari likiingia eneo hilo na ni kama vile alikuwa akilitambua gari hilo ni la boss wake. Alishangaa kwa sababu walivyoachana na mama Vannesa boss huyo alieleza kuwa amefika nyumbani kutoka Mwanza kwenye semina.
Ilimlazimu kusimama maana alihisi kama amefananisha hilo gari. Kwa kuwa yeye alikuwa gizani hakuwa na hofu sana maana mtu alaiye kwenye mwanaga ilikuwa ni ngumu sana kumwona. Alishangaa kuona boss wake huyo akishuka na mwanamke mwingine ambaye na yeye hakuhitaji mwanga wa mchana kujua kama alikuwa ni mrembo. Alitamani hata kuwapiga picha lakini wahusika hao waliingia kwa haraka sana. Wazo lilomjia ni kumpigia simu mama Vanesa na kumuuliza kama mumewe alikuwepo nyumbani au la. Aliingia ndani na kuchukua simu yake ambayo alikuwa ameiweka chaji. Alipiga namba za mama Vannesa lakini kwa bahati mbaya simu hiyo haikupokelewa. Haikuwa usiku sana lakini alishindwa kupiga tena kwa imani kuwa huenda ni usiku na yupo na mumewe. Aliamua kuamini kuwa alichokiona haikikuwa sahihi na zaidi ilikuwa ni hisia zake tu. Alitamani kwenda mpaka kwenye ile lodge lakini alikuwa na hofu huenda akaanza kuulizwa maswali mengi na mlinzi.
ITAENDELEA………………………………….
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni