Jumatano, 2 Oktoba 2019

DARASA* *HURU

**

Itifaki - ni mpangilio au utaratibu wa mambo uliowekwa na Watu au taasisi fulani.
Itifaki ya Chama cha Mapinduzi - ni mpangilio au utaratibu wa kuendesha , kupanga au kupangilia mambo ya Ccm au shughuli mbalimbali za Chama.
Pia Itifaki ndani ya Ccm ni sehemu ya kanuni zilizokubalika na kutumika katika Chama mara baada kupitishwa na Halmashauri kuu ya Taifa.
Chama cha Mapinduzi kinaongozwa na Katiba , kanuni, Miongozo , Taratibu na Maelekezo toka ( Waraka nk ) kutoka Makao Makuu.
Itifaki nyingi hazipo katika Katiba , hazipo katika Kanuni wala hazipo katika Miongozo,  isipokuwa zipo katika taratibu na Waraka mbalimbali za Chama.
Mfano: Itifaki ya Ukaaji katika Mikutano ya Chama, huwezi kuona katika Katiba, huwezi kuona katika Kanuni lakini Chama kina Itifaki ya ukaaji , yaani nani akae wapi na kwa nafasi gani , au Itifaki ya Utambulisho katika Chama nani aanze na nani wa mwisho kutambulishwa katika watu waliohudhuria eneo hilo.
Itifaki nyingi za Chama hazifahamiki na Wanachama na Viongozi kwa kuwa Wanachama au Viongozi wengi hutegemea kupata mambo mengi Katika Katiba na Kanuni tu, wanasahau kuwa kuna Taratibu, miongozo na Waraka mbalimbali zinazoendesha Chama cha Mapinduzi.
Leo nitazungumzia *Itifaki* *ya* *Mikutano* *tu*
Itifaki ya ukaaji katika Mikutano ya Chama cha Mapinduzi imegawanyika katika sehemu kuu zifuatazo :-
*1* *.* *JUKWAA*
*2* *.* *HADHIRA*

Tuanze na *JUKWAA*
Eneo hili ni sehemu ya mbele ambayo Viongozi wa Mkutano pamoja na wageni (Rasmi) hukaa. Sehemu katika Chama imezoeleka kuitwa meza kuu. Sehemu hii Viongozi hukaa kutokana na nafasi (vyeo ) walivyonavyo katika kupata mpangilio wa ukaaji meza kuu.
Utaratibu wa ukaaji meza kuu ni kwamba Mwenyekiti wa Kikao hukaa kiti cha Katikati mwa Meza Kuu, Katibu wa Kikao atakaa mkono wa Kushoto wa Mwenyekiti , Katibu Mwenezi ( kama kikao ni cha Chama au Mhamasishaji kama kikao cha Vijana au Katibu Malezi kama kikao ni cha Wazazi ) atakaa pembeni ya Katibu ( kushoto ) , Wajumbe wengine wa Kamati ya siasa au Kamati ya Utekelezaji watakaa pembeni kulia na kushoto kwa ku-balance meza isizidi sana upande mmoja.
Ukaaji huu ni kwa vikao visivyo Kamati za Siasa na Kamati za Utekelezaji.
*Endapo* *kikao* *hiki* *kitakuwa* *na* *Mgeni* *rasmi* *na* *Msafara* *wake* Mgeni rasmi atakaa kiti cha  katikati mwa meza kuu , mkono wa kushoto wa Mgeni rasmi atakaa Mwenyekiti wa Kikao husika , mkono wa kushoto wa Mwenyekiti wa Kikao watakaa wenyeji yaani Katibu nk. Mkono wa kulia wa Mgeni rasmi watakaa aliofutana nao kwa kuzingatia vyeo vyao.
Ikumbukwe idadi ya viti vya meza kuu mstari wa kwanza visizidi kumi na moja, kama wageni na Viongozi wenyeji watakuwa wamezidi watakaa mstari unaofuata, kama hakuna nafasi ya kupanga mstari mwingine vitapangwa viti eneo la mbele mbele karibu na meza kuu kwa kufuata utaratibu wa kushoto Wenyeji na kulia wageni.
*2* *.* *HADHIRA*
Eneo hili ni sehemu wanayokaa wajumbe mbalimbali wa kikao / mkutano ambao watakaa kwa kuangalia meza kuu.
Eneo hili itifaki inatutaka kukaa kwa kuzingatia uwakilishi wa maeneo tunayotoka, mfano wajumbe watakaa Kimkoa , kiwilaya, kikata, kimatawi au kimashina.
*UINGIAJI*
Itifaki ya uingiaji katika Vikao/ Mikutano wanatangulia Wajumbe kabla ya Mwenyekiti / Mgeni Rasmi
*NYIMBO* *ZA* *KUINGILIA*
Sio kila nyimbo ya Chama inatumika kuingiza Viongozi katika Vikao, kwa vikao vya Chama nyimbo inayotumika kuwaingiza Viongozi ni *"* *Chama* *chetu* *cha* *Mapinduzi* *chajenga* *Nchi* *”*
Umoja wa Vijana nyimbo ya kuingiza Viongozi katika  Vikao ni " *Eee* *Vijanaa* , *Vijana* , *Vijana* *tayarii* , *kulitumikia* *Taifa* , *Taifa* *Tanzania* ”
Asanteni sana , naomba niishie hapo tutaendelea kujuzana mengine.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni