Jumatatu, 25 Februari 2019

MAUAJI YALIYOJAA UTATA 2

*MAUAJI YALIYOJAA UTATA*

*Sehemu ya Pili  (2).*

“You are a killer,” (Wewe ni muuaji)
“No! I am not a killer officer, I am not,” (Hapana! Mimi si muuaji ofisa, mimi si muuaji)
“You killed them, why? Why did you kill them? Why?” (Umewaua, kwa nini? Kwa nini umewaua? Kwa nini?)
“I killed nobody officer,” (sijamuua yeyote ofisa)
Yalikuwa ni mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea ndani ya chumba kimoja katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini New York. Ndani ya chumba kile, kulikuwa na kijana mmoja, kwa kumwangalia, alikuwa na miaka isiyozidi ishirini na tano, alikuwa mtu mwenye mchanganyiko wa rangi, mama yake alikuwa Mzungu na baba yake alikuwa mtu mweusi.
Polisi wanne waliovalia makoti makubwa ambayo nyuma yaliandikwa NYPD yaani New York Police Department walikuwa wakifanya naye mahojiano kwa sauti kubwa, walimuuliza maswali na kumwambia kwamba yeye alikuwa muuaji lakini alikataa, alikataa katakata lakini polisi hawakuacha, waliendelea kumwambia kwamba alifanya mauaji.
Polisi hao walizungumza naye kwa zaidi ya dakika arobaini, neno lao lilikuwa lilelile kwamba mtu huyo alikuwa muuaji. Kijana huyo aliyeitwa Benjamin Saunders hakukubali, aliwaambia wazi kwamba hakuwa amemuua mtu yeyote na katika maisha yake hakuwahi kuua hata siku moja.
Polisi hawakuridhika, waliendelea kumwambia hivyohivyo mpaka baada ya dakika kadhaa walipotoka ndani ya chumba hicho. Benjamin alikuwa kimya, pingu zilikuwa mikononi mwake, alilia, kila alipokiangalia kile chumba, moyo wake ulimuuma mno, hakuwahi kufikiria kwamba kuna siku angeitwa ndani ya jumba hilo kubwa la polisi na kuambiwa kwamba aliua.
Wakati akiwa humo huku akilia, mara mlango ukafunguliwa, wanaume wawili waliovalia suti nyeusi wakaingia ndani, mmoja alikuwa na begi dogo, wakachukua viti na kukaa mbele yake.
Hawakuzungumza kitu kwanza, walibaki wakimwangalia kwa muda, waliporidhika, wakachukua vitambulisho vyao na kumuonyeshea Benjamini, walikuwa ni maofisa kutoka katika Shirika la Kijasusi la FBI(Federal Bureau of Investigation).
“Naitwa Brett Phillip,” alisema mwanaume mmoja.
“Naitwa Ryan Cashman,” alisema mwingine na kunyamaza.
Benjamin akawaangalia wanaume hao usoni, walionekana kuwa makini na kazi yao. Walipoona kijana huyo ameangalia vitambulisho vyao na kujiridhisha kwamba wao walikuwa maofisa kutoka FBI, wakavirudisha vitambulisho vyao mifukoni.
“Tunajua kwamba hukuua, tunajua hilo Benjamin,” alisema Brett huku akimwangalia Benjamin usoni.
“Ndiyo! Sijaua, sijawahi kuua, na kamwe sitoua,” alisema Benjamin kwa sauti ya chini huku akijifuta machozi.
“Ila alama zote zinaonyesha kwamba uliua,” alisema Brett.
“Sijajua nini kilitokea ila sijamuua mtu yeyote,” alisema Benjamin.
“Kweli?”
“Ndiyo! Sijamuua yeyote yule.”
Alichokifanya Brett ni kuchukua begi lake aliloingia nalo humo ndani, akalifungua na kutoa karatasi fulani kisha kuiweka mezani huku akimtaka Benjamin aichukue na iangalie.
“Mungu wangu!” alisema Benjamin huku akianza kulia.
“Kweli mpaka hapo unasema hujaua?”
Benjamin akabaki kimya, kile alichokiona kwenye karatasi ile hakuamini, hakujua kitu gani kilitokea, mbele yake aliona giza na kuona maisha yake yakienda kuisha gerezani kama si kuchomwa sindano ya sumu au kunyongwa.
Mdomo wake ulikuwa mzito mno, hakuamini alichokuwa akikiangalia katika karatasi ile, akawaangalia maofisa waliokuwa mbele yake, walionekana kuwa makini na kazi zao, mtazamo waliokuwa wakiutumia kumwangalia Benjamin, ulionyesha walikuwa na uhakika kwamba kijana huyo alikuwa amefanya mauaji waliyokuwa wakimshuku.
“Una lolote la kujitetea kabla hatujakwenda mahakamani?” aliuliza Brett.
“Sikuwahi kufanya mauaji, sijui nini kilitokea...”
“Lakini alama zako zimekutwa kama ushahidi.”
“Najua, ila sijafanya mauaji......ninaanza kukumbuka, ninaweza kuwatajia aliyefanya mauaji haya, ila si mimi. Nakumbuka niliambiwa nifanye mauaji haya, nikakataa, nililazimishwa sana, niliendelea kukataa, nikaambiwa kwamba kama ninakataa, basi kuna mtu atafanya mauaji, baada ya hapo, nitaonekana mimi ndiye nimefanya mauaji. Mungu wangu! Kwanza mchumba wangu Vivian yupo wapi? Walimuua, kwa nini walimuua msichana ninayempenda?” aliuliza Benjamini huku akilia.
Maofisa wale walibaki wakimwangalia, alionekana kukumbuka kitu, kwa jinsi alivyokuwa akijitetea, hata muonekano wake ulionyesha kabisa kwamba hakuwa amefanya mauaji. Kitendo cha kusema kwamba alimfahamu muuaji, kwa maofisa hao kilionekana kuwa nafuu kwao, hicho ndicho kitu walichokuwa wakikihitaji kwani kwa jinsi mauaji yalivyokuwa yamefanyika, ilikuwa ni vigumu kumgundua muuaji.
“Sawa! Sasa muuaji ni nani?” aliuliza Brett huku yeye na mwenzake wakimwangalia Benjamin usoni.
****
Julai 4, 2010
Washington DC
Zaidi ya watu elfu tatu walikuwa wamekusanyika kwa wingi nje ya Ikulu ya Marekani, White House kwa ajili ya kusikiliza hotuba kutoka kwa rais wa nchi hiyo, Barack Obama ambaye ndiye alikuwa akitimiza mwaka wa pili tangu aingie madarakani na kuwa rais wa nchi hiyo.
Watu wote waliokuwa hapo, walikuwa na bendera za nchi yao, waliipenda, waliitukuza na kuiona kuwa na thamani kuliko nchi zote duniani.
Siku hiyo ya kusherehekea Uhuru wa nchi yao tangu mwaka 1776 ambapo George Washington aliuchukua kutoka kwa Waingereza, ndiyo siku ambayo Wamarekani wote duniani huithamini kuliko siku yoyote ile.
Wanafunzi hawakwenda shuleni, wanachuo hawakwenda vyuoni, wafanyakazi hawakwenda kazini, yaani kila mtu alitakiwa kukaa nyumbani kwake, kwa wale waliokuwa mbali na Jiji la Washington, walitakiwa kubaki nyumbani na kuangalia kila kitu kilichokuwa kikiendelea huko kupitia runinga zao ila kwa waliokuwa Washington tena waliokuwa na nafasi, walitakia kufika katika uwanja wa Ikulu ya Marekani, White House.
Miongoni mwa watu wengi waliokuwa katika eneo la uwanja wa Ikulu hiyo alikuwepo kijana msomi kutoka katika Chuo Kikuu cha Harvard, Benjamin Saunders ambaye alibakiza mwaka mmoja kabla ya kuhitimu masomo yake.
Benjamin hakuwa peke yake, alikuwa na mpenzi wake, Vivian ambaye alisafiri kutoka Los Angeles mpaka hapo Washington kwa ajili ya kumsikiliza rais wao mweusi ambaye alitaka kuzungumza na Wamarekani wote duniani.
Kama walivyokuwa wengine, hata na wao walikuwa na bendera za nchi hiyo mikononi mwao. Muda wote walikuwa wakishangilia, walionekana kuwa na furaha mno huku wakati mwingine wakikumbatiana, hakukuwa na kitu kilichowapa furaha kama kuwa wote katika kipindi kama hicho.
Walipendana mno, hakukuwa na kitu ambacho kingeweza kuwatenganisha. Japokuwa walikuwa kwenye mafarakano ya mara kwa mara lakini muda mwingi walionekana kuwa na furaha kana kwamba hakukuwa na kitu kibaya kilichokuwa kikiendelea.
“Tukitoka hapa?” aliuliza Vivian.
“Twende nyumbani!”
“Kwako?”
“Kwani unaogopa nini?”
“Siogopi chochote, ila naweza kuchelewa masomo,” alijibu Vivian.
“Wala usijali, utawahi tu,” alisema Benjamin.
Benjamin alikuwa akisoma katika Chuo Kikuu cha Harvard kilichokuwa jijini Cambridge ndani ya Jimbo la Boston hapohapo nchini Marekani, mbali na kutoka katika familia iliyokuwa na fedha, Benjamin alikuwa na uwezo mkubwa chuoni. Alikuwa akichukua masomo ya uuguzi, ndoto yake kubwa iliyokuwa mbele yake ni kuwa daktari bingwa wa magonjwa ya moyo nchini Marekani.
Hiyo ilikuwa ndoto yake, hakutaka kuiona ikipotea, katika maisha yake, alimuahidi mama yake kwamba kuna siku angekuwa daktari mkubwa wa magonjwa ya moyo nchini Marekani, baba yake alikufa kwa ugonjwa wa moyo, hakutaka kuona watu wengine wakifa na ndiyo maana alisoma sana kufanikisha ndoto hiyo aliyojiwekea.
Mpenzi wake alikuwa akisomea masomo ya uandishi wa habari katika Chuo cha UCLA (University of California, huko Los Angeles). Kama alivyokuwa Benjamin, hata naye Vivian alikuwa na uwezo mkubwa darasani, aliwaongoza wanachuo wenzake na kuonekana kufanya mambo makubwa hapo baadaye kupitia uandishi aliokuwa akiusomea.
“Ngriii...ngriii...ngriii...” ulisikika mlio wa simu ukiita, mbali na kuita, simu hiyo ilikuwa katika mtetemo.
Mlio wa simu hiyo waliusikia kwa mbali kutoka na kelele zilizokuwa mahali hapo lakini baada ya Benjamin kuhisi mtetemo huo kutoka mfukoni mwake, harakaharaka akaichukua simu hiyo.
Alishangaa, haikuwa simu yake lakini aliikuta katika mfuko wa koti lake, si yeye tu aliyeshangaa, hata msichana wake, Vivian alishangaa pia. Walibaki wakiangaliana kwa sekunde kadhaa, hawakujua ni nani aliiweka simu ile katika koti lake na wala hawakujua lengo la huyo mwekaji lilikuwa nini.
“Hiyo simu umeitoa wapi?” aliuliza Vivian.
“Sijui, ndiyo kwanza nimeikuta mfukoni mwangu!”
“Nani amekuwekea?”
“Sijui pia.”
“Hebu pokea.”
Alichokifanya Benjamin ni kuipokea simu ile na kuita. Japokuwa mtu wa upande wa pili alikuwa akizungumza lakini Benjamin hakuweza kumsikia kutokana na kelele zilizokuwa mahali pale.
Wakati akiwa na simu hiyo sikioni, mara wanaume wawili waliovalia suti wakamsogelea, wakaanza kumwangalia na kumshika mkono huku wakimtaka wamfuate.
“Kuna nini?”
“Wewe twende tu,” alisema mwanaume mmoja, Benjamin hakuwa na wasiwasi, akaanza kuwafuata kama alivyoambiwa, hata Vivian naye hakutaka kubaki mahali hapo, naye akaanza kuwafuata huku akionekana kuwa na hofu kubwa, kichwa chake kikaanza kujiuliza mambo mengi kuhusu watu wale, walikuwa wakina nani? Akakosa jibu.

JE, nini kitaendelea?

MAUAJI YALIYOJAA UTATA

*Sehemu ya Kwanza  (1).*

Ilikuwa ni taarifa mbaya, iliyoshtua ambayo ilianza kwa kusikika katika sehemu mbalimbali jijini Las Vegas nchini Marekani kabla ya kuwafikia polisi. Kila aliyezisikia taarifa hizo, hakuamini, wengi wakahisi kwamba hazikuwa taarifa za kweli, labda kulikuwa na mtu mwingine aliyetaka kuivumisha habari hiyo ambayo ilimsisimua kila mtu aliyeisikia.
Msichana mrembo aliyeitwa kwa jina la Stacie Lawrence, msichana aliyebahatika kunyakua taji la Urembo wa Dunia, alikutwa amekufa ndani ya chumba kimoja cha Hoteli ya Vikings Hill iliyokuwa Las Vegas, Nevada nchini Marekani alipokuwa amepanga huku akisubiri kuonana na Mkurugenzi wa Tovuti ya Google kwa ajili ya kusaini mkataba wa picha zake kutumika katika programu moja ambayo ingetumiwa katika simu zote zinazotumia system ya android.
Stacie aliyekuwa gumzo kwa kipindi hicho duniani kutoka na uzuriwake, alikutwa amekufa baada ya kujiovadosi madawa ya kulevya aina ya Heroine kwa kujichoma sindano katika mkono wake wa kulia wakati kitandani ndani ya hoteli hiyo.
Hiyo ndiyo ilikuwa habari ya mjini, kila aliyeisikia, hakuamini, swali la kwanza kabisa walilojiuliza watu ni juu ya utumiaji wa madawa ya kulevya. Kila mtu alijua kwamba Stacie hakuwahi kutumia madawa hayo, si kipindi hicho tu, hata kabla ya kutwaataji hilo, hakuwa mtumiaji, sasa ilikuwaje mpaka leo hii akutwe chumbani kitandani akiwa amejidunga madawa hayo? Hilo lilikuwa swali lisilokuwa na majibu.
Waandishi wa habari kutoka katika mashirika mbalimbali ya habari kama CNN, BBC, Sky News na hata wale wa kujitegemea tayari walikuwa nje ya hoteli hiyo, vitendea kazi vyao vyote vilikuwa mikononi mwao, walitaka kupiga picha na kupata habari kuhusu kifo cha msichana huyo mrembo ambaye bado uzuri wake ulikuwa gumzo duniani.
Polisi walitanda kila sehemu nje ya hoteli hiyo, mkanda wa njano ulioandikwa Do Not Cross yaani ‘Usivuke’ulizungushiwa katika hoteli hiyo kwa muda. Magari ya wagonjwa mawili yalikuwa yamekwishafika katika hoteli hiyo, kilichosubiriwa ni kuingia ndani na kuuchukua mwili huo.
Waandishi hawakuruhusiwa kabisa kuingia ndani ya hoteli hiyo, waliambiwa wasubiri hapo nje wakati polisi wakiingia ndani kwa ajili ya kufanya kazi yao, hawakuwa na la kufanya zaidi ya kusubiri.
Polisi wakaingia ndani ya chumba kile. Huko wakaukuta mwili wa Stacie ukiwa kitandani, katika mkono wake wa kushoto kulikuwa na sindano iliyochoma mshipa wake, aliishikilia kwa kutumia mkono wake wa kulia mbali na hivyo, pembeni yake kulikuwa na noti za Dola, Paundi, Yeni na Euro.
Udenda ulikuwa ukimtoka, pale alipokuwa, hakutingishika, kilikuwa kifo kibaya, kilichozua maswali mengi kwa watu wengi, maswali hayo yote, hakukuwa na mtu aliyekuwa na majibu zaidi ya Stacie mwenyewe ambaye kipindi hicho alikuwa marehemu.
“This is the fifth one, what the hell with the drugs?” (huyu ni mtu wa tano, kuna nini na haya madawa?) alisikika akiuliza mwanaume mmoja huku akionekana kushangaa.
“I don’t know. What the hell with these teenagers, they like to try each and every goddamn thing, why?” (sifahamu. Nini kinaendelea kwa hawa vijana, wanapenda kujaribu kila kitu, kwa nini?) aliuliza mzee mmoja huku akionekana kukasirika.
Kila mmoja alishangaa, huyo hakuwa mtu wa kwanza, supastaa aliyejiua baada ya kujiovadozi kwa madawa ya kulevya, huyo alikuwa mtu wa tano, kijana supastaa ambaye aliamua kujiua kwa kujidunga sindano ya madawa ya kulevya.
Mtu wa kwanza kabisa kujiua kwa kujidunga shindano alikuwa Paul McKenz. Huyu alikuwa mcheza kikapu aliyekuwa akichipukia, mwenye sura nzuri, alijitengenezea jina kubwa katika Timu ya La Lakers, akaanza kupata mashabiki wengi, alipendwa na kila mtu aliyekuwa akiupenda mchezo huo, jina lake likaanza kuwa kubwa, akapata mikataba mingi lakini mwisho wa siku, Paul akaja kujidunga sindano yenye madawa ya kulevya aina ya Methamphetamine chumbani kwake.
Watu wengi walisikitika kwani ndiye alikuwa kijana aliyekuwa akichipukia katika mafanikio makubwa. Hiyo haikuishia hapo, pia kulikuwa na kijana mwingine aliyekuwa na kipaji cha uigizaji. Katika filamu yake ya kwanza ya Fallen Tree, alishinda Tuzo ya Oscar, Global na nyingine nyingi, huyu aliitwa Todd Lewis.
Bahati ikaanza kuonekana upande wake, akapendwa sana, kila kona alisikika yeye tu. Kadiri jina lake lilivyovuma ndivyo alivyozidi kujitengenezea mashabiki. Wakati akiwa amenunua gari yake ya kwanza ya thamani kabisa aina ya Ferrari Testarossa nyekundu, akakutwa naye akiwa amejidunga madawa ya kulevya ndani ya gari lake nje ya klabu moja huku pembeni kukiwa na noti ya dola, paundi, Yuan na Euro. Watu walisikitika na kulia, vilio vyao, huzuni zao hazikuweza kuwarudisha watu hao duniani.
Mtu mwingine kabla ya Stacie kujiua kwa madawa ya kulevya alikuwa kijana aliyeitwa kwa jina la Carter Phillip. Huyu alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wakichipukia katika muziki wa Pop. Alikuwa na sauti kali, yenye nguvu ambapo kila alipokuwa akiitumia katika nyimbo zake, wanawake walichanganyikiwa.
Alikuwa mzuri wa sura, mwili uliojengeka. Kibao chake cha kwanza kabisa cha Come and Get Me Shawty alichokitoa kilitingisha kila kona duniani. Uwezo wake ulionekana, si hapo tu hata kwenye Shindano la American Got Talent, mpaka aliposhinda, watu waliona kipaji kikubwa ndani yake.
Wengi wakatabiri kwamba Carter ndiye angekuwa mrithi sahihi wa Michael Jackson, wengi wakamtabiria mema, njozi njema ikaonekana mapema kabisa kwani ngoma zake mbili alizozitoa, zote zilishika nafasi za juu kabisa katika orodha ya Billboard.
Akatengeneza fedha nyingi huku ndiyo kwanza akiwa na miaka kumi na tisa. Akapendwa, akawa kipenzi kikubwa cha watu ila baada ya kwenda nchini Uingereza kwenye Tamasha la UKIMWI lililokuwa likifanyika katika Jiji la Southampton, akakutwa akiwa amejiua ndani ya chumba alichochukua hotelini baada ya kujidunga sindano iliyokuwa na madawa ya kulevya aina ya Dextromethorphan huku pembeni kukiwa na noti za dola, paundi, yuan na euro.
Hakukuwa na aliyejua sababu ya vijana hao kujidunga madawa hayo ya kulevya, kila mtu aliyepata habari za vijana hao alishtuka. Mpaka katika kipindi ambacho msichana mrembo, Stacie kujiovadozi madawa hayo, bado watu hawakujua sababu ilikuwa nini, ni afadhali kama wangekuwa wamepigika katika maisha yao, ila kilichoshangaza, walikuwa wakianza kupata umaarufu, kupata fedha, na ndipo kipindi hichohicho nao waliamua kujidunga madawa ya kulevya.
Dunia ikatetemeka, watu wakaogopa kuwa mastaa, wengi walisikia kwamba unapokuwa staa, ilikuwa ni lazima kutumia madawa ya kulevya. Wazazi walipowaona vijana wao wanaanza harakati kupitia vipaji vyao, waliwazuia kwa kuona kwamba mwisho wa siku wangejiua kama hao wengine.
Swali kubwa ambalo waandishi wa habari walihoji, mitaani ni sababu gani zilizopelekea vijana hao kujidunga madawa ya kulevya? Kila aliyeuliza swali hilo, alikosa jibu kabisa.

Je, nini kitaendelea?
Nini kilipelekea watu hao, mastaa wakubwa kujimaliza kwa kujiovadozi madawa ya kulevya?

Tukutane ....

Jumatano, 20 Februari 2019

Teaching methods and classroom management.

Teaching methods and classroom management.

Uingiapo darasani kumbuka kuandika tarehe upande wa kulia juu ya ubao, gawa ubao x 3 na andika heading ya somo sehemu ya katikati juu ya ubao.
Andaa lesson plan vizuri ili iwe ni kiongozi wako kujuwa uliachia wapi na unaanzia wapi, haitakiwi kwa mwalimu kuwauliza wanafunzi KIPINDI KILICHOPITA TULIISHIA WAPI!! mwalimu wa namna hiyo inaonekana kabisa haandai lesson plan na inabidi afukuzwe kazi haraka Sana.

Mwalimu tumia sana njia ya kuwashirikisha wanafunzi katika kuelezea baadhi ya mambo LEARNER CENTERED ili kujuwa uwezo wa wanafunzi pia unaweza kwa njia hi kujifunza baadhi ya taaluma kutoka kwa wanafunzi.

Mwalimu uwapo darasani hakikisha kabisa unazima simu yako kwani ni makosa kwa mwalimu kupokea au kupiga simu wakati akiwa katika kipindi darasani kwani hii husababisha pia kutafuna muda wa kipindi ambao tayari umeshakadiriwa kwa kila dakika katika lesson plan.

Mwalimu unapokuwa darasani jitahidi kujuwa majina ya wanafunzi wote kwani haipendezi kumuita mwanafunzi WEWE.

Mwalimu uwapo darasani ni lazima ujuwe wanafunzi wenye akili sana na slow learners na unapofundisha wazingatie zaidi wale ambao uelewa wao ni mdogo.

Mwalimu uwapo darasani kuwa mcheshi na jenga urafiki na utani usiopindukia mipaka kwa wanafunzi wote wajenge wanafunzi wakuheshimu wasikuogope.

Mwalimu uwapo darasani epuka kuwakatisha tamaa wanafunzi waliokosea kujibu maswali au kushindwa kusomo vizuri Bali wapongeze sana kwa kujaribu na tumia njia bora ya kuwasahihisha.

Mwalimu uwapo darasani usichague wanafunzi haohao tu kujibu maswali hi inapelekea wengine kujiona hawana umuhimu.

Mwalimu unapomaliza kipindi darasani ni Bora kuwafahamisha wanafunzi topic ijayo ili wanafunzi wajiandae nayo.

Mwalimu uingiapo darasani hakikisha una teaching instruments kama chaki, rula, ufutio nk, epuka kuwatuma wanafunzi chaki na kadhalika kwani kufanya hivyo kunatafuna kipindi chako ambacho kimewekewa muda maalumu.

Kwa leo tuishie hapa tutaendelea Kesho Inshallah.

Jumapili, 17 Februari 2019

WATANZANIA VS WANA WA ISRAEL.

WATANZANIA VS WANA WA ISRAEL.

Na Thadei Ole Mushi.

Kilichowachelewesha wana wa Israel kufika nchi ya ahadi toka utumwani ni masikilizano tu. Kutoka Misri hadi Israel hazifiki KM 700. Lakini walitumia muda wa miaka 40 kufika Israeli. Musa alienda kuwaokoa akiwa kijana kabisa lakini alizeekea njiani na kufa kabla hajafika Israel. Kama walikuwa wanasikilizana wangetumia hata nusu ya mwaka wangefika. Lakini walikuwa wanafika mahali wanaanza kulaumiana,kugombana na hata kumkufuru Mungu kwa matendo yao.

NATAKA KUSEMA NN?

1. #Hili swala la Korosho wakati linaanzia Bungeni kwa wabunge wa kusini kulalamikia Fedha ya makato ya Korosho kutokurudishwa kwa wakulima Mimi nilichagua upande na nikasimama na kina Nape.

Wengine wakasimama na Mpango, wakati wa kuhitimisha kikao cha Bunge waliosimama na Mpango wakashangilia huku Mpango akijinasibu kuwa hakuna wa kumzuia kwenda Mtwara na Lindi.

Nikitahadharisha kuwa mjadala haukufungwa Bali utahamia mtaani watu hawakunielewa.

2. #Wakati Serikali inapiga Marufuku ununuzi wa Korosho kwa kutumia mtindo wa Kangomba niliibuka tena nikasema kuna watu watafilisika kwa kuwa hawa walikopa kwa ajili ya kuwa Middle Man katika biashara ya Korosho. Hakuna biashara isiyokuwa na Broker. Huu ni utaratibu wa kawaida kabisa kwenye biashara.

Tumefilis watu waliokuwa wanafanya biashara ya Kangomba na Bado Tumeshindwa kuimaliza Korosho na mkulima ameendelea kuteseka.

3. Sasa Tumehamia kwenye Indo Power, Ni Korosho ile ile iliyoanzia Bungeni Mwaka Jana.

Gazeti la Mwananchi Jana limeripoti kuwa Indo hawana Hata account bank. Kwa maana hiyo hawa hawana tofauti na waliokuwa wanafanya biashara ya Kangomba.

Kwa maana Rahisi tumekataa mabroker wakwetu Tanzania tukakubali mabroker toka Kenya.

Tatizo ni kutokusikilizana tu.

Tufike mahali Ndani ya Serikali tuwe na kitengo cha kuchuja michango ya watu mbalimbali. Si vibaya kukubali ushauri toka kwa upinzani.

Kazi kubwa ya Upinzani pamoja na kuwa wanaitaka Dola waiongoze lakini kazi yao nyingine ni kutoa mawazo mbadala. Tujenge utamaduni wa kuyaheshimu mawazo yao.

Ole Mushi

Ijumaa, 15 Februari 2019

MEDICAL ADVISE

MEDICAL ADVISE 💗

           HIGH BP
          ----------
120/80 --  Normal
130/85 --Normal  (Control)
140/90 --  High
150/95 --  V.High
----------------------------

           PULSE
          --------
72  per minute (standard)
60 --- 80 p.m. (Normal)
40 -- 180  p.m.(abnormal)
----------------------------

          TEMPERATURE
          -----------------
98.4 F    (Normal)
99.0 F Above  (Fever)

Please help your Relatives, Friends by sharing this information....

Heart Attacks And
Drinking Warm
Water:

This is a very good article. Not only about the warm water after your meal,
but about Heart Attack's . The Chinese and Japanese drink hot tea with their
meals, not cold water, maybe it is time we adopt
their drinking habit while
eating. For those who like to drink cold water, this
article is applicable to
you. It is very Harmful to have Cold Drink/Water during a meal. Because,
the cold water will solidify the oily stuff that you
have just consumed. It will
slow down the digestion. Once this 'sludge'
reacts with the acid, it will break down and be
absorbed by the intestine faster than the solid food. It will line the intestine. Very soon, this will turn into fats
and lead to cancer . It is best to drink hot soup
or warm water after a meal.

French fries and Burgers
are the biggest enemy of heart health. A coke after that gives more power to
this demon. Avoid them for
your Heart's & Health.

Drink one glass of warm water just when you are about to go to bed to avoid clotting of the blood at night to avoid heart attacks or strokes.

A cardiologist says if everyone who reads this
message sends it to 10 people, you can be sure that we'll save at least one life.
Cheers And Enjoy life

💉BLOOD GROUP COMPATIBILITY

Compatible Blood Types

O- can receive O-

O+ can receive O+, O-

A- can receive A-, O-

A+ can receive A+, A-, O+, O-

B- can receive B-, O-

B+ can receive B+, B-, O+, O-

AB- can receive AB-, B-, A-, O-

AB+ can receive AB+, AB-, B+, B-, A+,  A-,  O+,  O-

This is an important msg which can save a life! A life could be saved..
EFFECT OF WATER                 
💐 We Know Water is
       important but never
       knew about the
       Special Times one
       has to drink it.. !!

       Did you  ??? 

💦 Drinking Water at the
       Right Time ⏰
       Maximizes its
       effectiveness on the
       Human Body;

       1⃣  1 Glass of Water
              after waking up -
             🕕⛅ helps to
              activate internal
              organs..

       2⃣  1 Glass of Water
              30 Minutes  🕧
              before a Meal -
              helps digestion..

       3⃣ 1 Glass of Water
              before taking a
              Bath 🚿 - helps
              lower your blood
              pressure.

       4⃣ 1 Glass of Water
              before going to
              Bed - 🕙 avoids
              Stroke  or Heart
              Attack.

      'When someone
       shares something of
       value with you and
       you benefit from  it,
       You have a moral
       obligation to share it
       with others.

PREPOSITIONS ATTACHED TO CERTAIN WORDs

Help your child master.PREPOSITIONS ATTACHED TO CERTAIN WORDs

1.abide..............by
2.absorbed....... In
3.abstain ......from
4.Accomplice......with
5.accused...... (Sb)of(sth)
6.accustomed..... To
7.addicted........ To
8.adhere........ To
9.admit........to/into
10.advantage....... Over (sb) of (sth)
11.advantage........ Of(sth)
12.affection.......... For
13.afflicted......,. With
14.afraid......... Of
15.agree.......... To(proposal)
16.agree............. With(a person)about/on sth
17.aim .......at
18.aloof........from
19.alternative......... To
20.amazed.......... At
21.angry............with/at(sb)
22.angry............at/about(sth)
23.anxious.......... For(sb)
24.anxious........ About (sth)
25.apologize...... To(sb) for (sth).
26.appeal........ To(sb)for(sth)
27.appetite..... For
28.approach........to
29.akin........to
30.acclimatize........ To
31.apparent........ To(sb)
32.apparent...... From(sth)
33.appoint.......(sb)to(sth)
34.apply........ To(sb)for(sth)
35.appropriate........ To/for
36.approve..............of
37.aptitude............ For
38.ashamed............ Of
39.aspire...................to
40.assent..................to
41.associate..........with
42.dissociate........from
43.assure...............of
44.astonished........ At
45.atone................. For.
46.attached..............to
47.attend..................to
48.attribute......(sth) to (sth/sb)
49.authority........Over(=power)
50.authority............ On(=expert)
51.avail.........(oneself)of(sth)
52.averse.................to
53.ban(n)..............On
54.ban(v)...........(sb)from(sth/doing sth)
55.bad..........at(=not good at)
56.bad............for(=harmful)
57.believe.............in
58.beneficial................ To
59.benefit................ By/from
60.blame.............(sb/sth)for(sth).
61.boast................of
62.bound............... For
63.burden(n)............... To
64.burden(v)................with
65.busy.................with
66.bearing.............. On
67.campaign........... Against/for
68.capable............... Of
69.concern.............. For/about
70.careful...............about/for
71.caution............ About/against
72.charge.............. With
73.claim..................on/to
74.clash........... With(sb)over(sth)
75.collide................with
76.Collude.........with(sb)in(sth)
77.comment................on
78.compare..........to(=to show likeliness)
79.compare ..............with(=to show contrast)
80.compassion.......... For
81.compatible........... With
82.compensation....... For
83.compliance............ With
84.compliment............. On
85.comply................. With
86.conducive............. To
87.confide.............in(=trust)
88.confide.............to(=tell)
89.confidence.............In. 
90.confident............. Of/about
91.confined.......... (Sb/sth)to(sth)
92.conform............ To
93.conformity......... With
94.congenial............. To
95.congratulate......... (Sb)on(sth)
96.connect.......(sth)to(sth)
97.consent............. To
98.consist................of
99.contemporary........ With
100.contempt........... For
101.contend....... With(=to have to deal with a problem or difficult situation)
102.contend.........for(=to compete against sb  in order to gain sth)
103.content..............with
104.contrary.............to
105.control............ Over
106.connive..........at/in(sth)
107.connive..............with(sb)
108.close...................to
109.complain.........to(sb)about/of(sth)
110.crash...............into
111.convenient......... For(sb/sth)
112.converse.............. With
113.convict........... (Sb)of(sth)
114.cure(v).......(sb)of(sth)
115.cure(n).............for
116.concern(n)........about/for/over.
117.concerned (adj)........about/for/over(=worried)
118.concerned (adj).......about/with(=interested in)
119.deal........in(=trade)
120.deal.......with(=to take appropriate action).
121.delight.................in
122.depend......... On/upon
123.deprive..........(sb/sth)of(sth)
124.desist............... From
125.destitute................of
126.detrimental............ To
127.deviate................ From
128.devoid................. Of
129.differ........
..from(sb/sth)=to be different from sb/sth
130.differ............with(sb) about/on/over (sth)=to disagree with SB
131.different........... From/to/than
132.disgusted.......... At/by/with
133.dispense............ With
134.dispose.............of
135.die.......................of
Eg:person died of accident.

Die.........with(=disease)
Eg: person died with cancer

Die.............for(=purpose)
Eg:person died for country/organization.
136.dissent..........from
137.dote........... On/upon
138.double (n)/doubtful (adj)........about
139.drenched....... In/with
140.decline......... In/of
141.eager................. For
142.eligible............... For
143.engaged......... In/on(sth)=busy doing sth
144.engaged....... To(sb )=having agreed to marry sb
145.enthusiasm.......... For/about
146.entrust......(sb)with(sth)
147.entrust.......(sth)to(sb)
148.envious/jealous......Of
149.envy...............at
150.entitle/entitlement.....To
151.equal........... To
152.escape......... From
153.essential........ To/for
154.excel..............at/in
155.exception.............. To
156.excuse.......... (Sb) for (sth)=forgive
157.excuse........ For (=reason)
158.exemption.......... From
159.expose.........(sth)to (sb)
160.encroach..........on/upon
161.expect....... (Sth)from (sb)
162.fail. ...............in
163.faith................. In
164.faithful............. To
165.famous........... For
166.fearful.............. For (sb)
167.fearful.............. Of(sth)
168.feed/live.....on(=eat)
169.fight....... With(sb)about/for (sth)
170.fill .........(sth)with(sth).
171.fill....................in(sth)
172.fit/unfit..............For
173.fond.....................of
174.fondness............ For
175.free............from/of
176.frightened............ At
177.full.......................of
178.fuss...........about/over
179.fed up..............with
180.glad.......about (=happy)
181.glad.......of(=greatful)
182.glance............... At
183.good......at(=able to do sth well)skillful
184.good.........for(=suitable) convenient
185.grapple........... With
186.greatful.......to(sb)for(sth)
187.grief........... At/over
188.grieve.........for/over
189.guard.........Against
190.guilty........ About
(=feeling ashamed because you have done sth that you know is wrong)
191.guilty........ Of(=having done sth illegal)
192.harmful/injurious.....To
193.heir...........to ( sth)
194.heir..........of (sb)
195.hint.............at
196.hope........... For
197.hope...........for/of
198.hopeful........... About/of
199.hostile............. To
200.habit......of(doing sth)
201.identical....... With
202.ignorant......... About/of
203.impact..... Of(sb)on(sth/sb)
204.impose........... On
205.impress....... (Sb) with(sth)
206.impression......... On(sb)
207.impression..... Of(sth)
208.impressed........with/by
209.independent........ Of
210.indifferent/callous......to
211.indispensable...... To(sb/sth)
212.indispensable........ For(doing sth)
213.infected................ With
214.infer....................from
215.influence..... Over(=control)
216.influence........ On/upon(=effect)
217.inform.............. Of
218.inquiry............about/into
219.insight............ Into
220.insist.................on
221.insistence..........on
222.interact.............. With
223.interaction......... With (sb/sth)
224.interaction....... Between (two things or persons)
225.interested........... In
226.interfere......... In(=get involved)
227.interfere........ With(=prevent)
228.invest....................in
229.involved...............in
230.irrelevant............... To
231.irrespective........... Of
232.meddle............... In
233.keen......................on
234.kind/cruel............to
235.lack....................of
236.lacking................in
237.lament...........over
238.laugh................. At
239.lead.....................to
240.leave..........for(a place)=go to
241.liable....... For(=legally responsible for paying the cost of)
242.liable........ To(=likely to be punished by law for)
243.listen............. To
244.longing (n)/long(v)..........for
245.look/stare/gaze.......at
246.lust.....................for
24
7
.march................on
248.married..............to
249.marvel................at
250.meditate/concentrate......on
251.mourn................. For
252.nag.....................at
253.need/necessity....For
254.negligent............. In
255.nervous........About/of
256.notorious.......... For
257.obedient............. To
258.object/objection.....to
259.oblige.....(sb)with(sth)
260.obliged..... To(sb)for (sth)
261.obsession..........with
262.obsessive.......... About
263.open...... To(sb/sth)
264.opportunity......for(sb/sth)
265.opportunity......for/of(doing sth)
266.part........from(=leave sb)
267.part......with(=to give sth to sb else)
268.partial............... To
269.partially.........For(sth)
270.passion..............for
271.pertain................to
272.persist..........in(doing sth)
273.persist........in/with(sth)
274.pleased...........With
275.pleasing........... To
276.popular............. With
277.pray......to(sb)for(sth)
278.prefer...... (Sb/sth)to(sb/sth)
279.preferable............. To
280.pretext...............for
281.prevail......on(=persuade)
282.prevail.......over(=defeat)
283.prevent.......... From
284.pride............. In
285.prior............... To
286.prohibit..........from
287.prone................ To
288.proud............... Of
289.provide..... (Sb)with(sth)
290.provide......(sth)fo(sb)
291.pessimistic....... About
292.positive...........About
293.quarrel........About(sth)
294.quarrel....... With(sb)
295.ready............ For
296.reconcile..... To(sth)
297.reconcile..... (Sth)with(sth)
298.recover(v).......from
299.recovery(n)......from
300.refer............... To
301.reference.......... To
302.rejoice.......... At/over
303.related............... To
304.rely...................on
305.remind..............of
306.remorse.......... For
307.request............for
308.resemblance..... To
309.resolve...............on
310.responsible.....for (sth)
311.restricted........ To
312.rid....................of
313.rob....................of
314.resign............ From
315.search................ For
316.seek..............for
317.senior/junior.......To
318.sensitive...... To/about
319.sequel................to
320.short...................of
321.similar................ To
322.smile/sneer/giggle...At
323.sorry.........about/for
324.spend.............on
325.stick...... To(=to continue doing sth despite difficulties)
326.subject............. To
327.submission........to
328.suffuse.............with
329.succeed.............. In
330.succession........in
331.succumb...........to
332.suffer.................from
333.superior/inferior......to
334.supplement.......... To
335.supply....... (Sth)to (sb)
336.supply.......(sb)with(sth )
337.surprised/shocked....At
338.suspect.......(sb/sth)of(sth)
339.suspicious............. Of
340.sympathize.....with(sb/sth)
341.thankful ......for(sth)
342.thankful............. To(sb)
343.thirst/hunger/desire.........For
344.threaten......(sb)with(sth)
345.tired..................... Of
346.stick................... Of
347.tremble.......... With
348.true..................to
349.used.................to
350.victory...... Over/against. 351.venue............. For
352.wait.................for
353.want.................of
354.waste............on(sth)
355.withdraw..........from
356.wonder...... About (=think about)
357.wonder......... At(=be surprised)
358.worthy............... Of
359.write...... (Sth)to(sb)
360.write..... In(ink/pencil)
361.write........ With(a pen)
362.yearn..............for
363.yearning............ For
364.yield.................. On
365.yield...............  VG.....to
366.thrive................... On
367.self-sufficient........inm
368.debate....... On/about/over
369.divergence.......between

Hillbridge college
ENGLISH Clinic
Changing the way the learners learn

Jumatatu, 4 Februari 2019

CURRICULUM VITAE

1.full name: ....................
2.date of birth: ................
3.place of birth: ...............
4.nationality: ..................
5.language: ................
6.marital status: ............
7.phone no: ..............
8.official address: ........
9.e mail address: ........
10.educational qualifications: ................
11.other courses/seminars attended: .........
12. date of first appointment: ..........
13.date of confirmation: ..........
14.present designation and salary scale: .............
15.date of first appointment to present grade: ...........
16.work experience: .............
17.areas of expertise: ...........
18.present station: .............
19.referees: ...................
20.file no.: ................

name:............. date ......... signature..............