Jumatatu, 17 Septemba 2018

MAKUNDI YA DAMU

MEDICAL FITNESS_

           *BLOOD PRESSURE*
          ----------
120/80 --  Normal
130/85 --Normal  (Control)
140/90 --  High
150/95 --  V.High
----------------------------

           *PULSE*
          --------
72  per minute (standard)
60 --- 80 p.m. (Normal)
40 -- 180  p.m.(abnormal)
----------------------------

          *TEMPERATURE*
          -----------------
98.4 F    (Normal)
99.0 F Above  (Fever)

*BLOOD GROUP COMPATIBILITY*

What’s Your Type and how common is it?

*O+*       1 in 3        37.4%
(Most common)

*A+*        1 in 3        35.7%

*B+*        1 in 12        8.5%

*AB+*     1 in 29        3.4%

*O-*        1 in 15        6.6%

*A-*        1 in 16        6.3%

*B-*        1 in 67        1.5%

*AB-*     1 in 167        .6%
(Rarest)

*Compatible Blood Types*

O- can receive *O-*

O+ can receive *O+, O-*

A- can receive *A-, O-*

A+ can receive *A+, A-, O+, O-*

B- can receive *B-, O-*

B+ can receive *B+, B-, O+, O-*

AB- can receive *AB-, B-, A-, O-*

AB+ can receive *AB+, AB-, B+, B-, A+,  A-,  O+,  O-*

This is an important msg which can save a life! A life could be saved...
What is ur blood group ?
Share the fantastic information..

*EFFECT OF WATER*                 
We Know Water is
       important but never
       knew about the
       Special Times one
       has to drink it.. !

       *Did you know ?*

  Drinking 1 Glass of Water at the Right Time Maximizes its effectiveness on the  Human Body;

         *1 Glass of Water*
              after waking up -
              helps to
              activate internal
              organs..

         *1 Glass of Water*
              30 Minutes  
              before a Meal -
              helps digestion..

        *1 Glass of Water*
              before taking a
              Bath  - helps
              lower your blood
              pressure.

        *1 Glass of Water*
              before going to
              Bed -  avoids
              Stroke  or Heart
              Attack.

      'When someone
       shares something of
       value with you and
       you benefit from  it,
       You have a moral
       obligation to share'

Jumanne, 4 Septemba 2018

SHAIRI KUHUSU WALIMU NA VIBOKO

Enyi  wenzangu walimu,
pole kwa haya mashaka,
Ule wetu umuhimu,
nchini umefutika,
Daima kutulaumu,
Kila kukipambazuka,
Walimu viboko sumu,
Tusichape ni mashaka,

Viboko sasa ni sumu,
Tusichape ni mashaka,
Ingawa hiyo nidhamu,
ya wanetu itashuka,
Kwa taifa hili bomu,
hatari likilipuka,
Walimu viboko sumu,
Tusichape ni mashaka,

Sisi ni wataalamu,
walimu siyo vibaka,
Walezi wenye elimu,
watu wa kuheshimika,
Kukosea si wazimu,
vipi tunadhalilika?
Walimu viboko sumu,
Tusichape ni mashaka.

Tusiache kujihimu,
Shuleni kuwajibika,
Iwe mwalimu wa zamu,
wa darasa kadhalika,
Wana tusiwahukumu,
Tukwepe kuwatandika,
Walimu viboko sumu,
Tusiwachape mashaka.

Watoto wanaharamu,
wale wasiyoonyeka,
Tusijipe kazi ngumu,
ya kuwafundisha nyoka,
Tumekuwa mahasimu,
Kundi liso thaminika,
Walimu viboko sumu,
Tusichape ni mashaka.

Kila kosa la mwalimu,
pale linapofanyika,
Yeyote huwa hakimu,
Makosa kuyabambika,
Tuelewe tufahamu,
Taifa limetuchoka,
Walimu viboko sumu,
Tusichape ni mashaka.

Malipo hii awamu,
nyongeza hawajaweka,
Maisha bado magumu,
pato halijanyanyuka,
Tukichapa washutumu,
Kwamba tumekasirika,
Walimu viboko sumu,
Tusichape ni mashaka.

Tumpe pole binamu,
Mwalimu alohusika,
Kwa ile adhabu ngumu,
Ajira kumponyoka,

BIOLOGY'S SOURCE

A SUMMARY OF HUMAN BIOLOGY
1: Number of Bones 206
2: Number of Muscles 639
3: Number of Kidneys 2
4: Number of Milk Teeth 20
5: Number of Ribs 24 (12 pair)
6: Number of Heart Chamber 4
7: Largest artery Aorta
8: Normal blood pressure 120/80mmHg
9: Ph of Blood 7.4
10: Number of vertebrae in the Spine 33
11: Number of vertebrae in the Neck 7
12: Number of Bones in Middle Ear 6
13: Number of Bones in Face 14
14: Number of Bones in Skull 22
15: Number of Bones in Chest 25
16: Number of Bones in Arms 6
17: Number of Muscles in Human Arm 72
18: Number of Pumps in Heart 2
19: Largest Organ Skin
20: Largest gland Liver
21: Biggest cell female Ovum
22: Smallest cell male Sperm
23: Smallest Bone Stapes
24: First transplanted Organ Heart
25: Average length of Small Intestine 7m
26: Average length of Large Intestine 1.5m
27: Average weight of new Born baby 2.6kg
28: Pulse rate in One Minute 72 times
29: Normal body temperature 37 C° (98.4 F°)
30: Average Blood Volume 4 to 5 liters
31: Life Span of RBC 120 days
32: Life Span of WBC 10 to 15 days
33: Pregnancy Period 280 days (40 week)
34: Number of Bones in Human Foot 33
35: Number of Bones in Each wrist 8
36: Number of Bones in Hand 27
37: Largest Endocrine gland Thyroid
38: Largest Lymphatic Organ Spleen
39: Largest part of Brain Cerebrum
40: Largest & Strongest Bone Femur
41: Smallest Muscle Stapedius (Middle Ear)
41: Number of Chromosome 46 (23 pair)
42: Number of Bones in new Born baby 306
43: Viscosity of Blood 4.5 to 5.5
44: Universal Donor Blood Group O
45: Universal Recipient Blood Group AB
46: Largest WBC Monocyte
47: Smallest WBC Lymphocyte
48: Increase RBC count called Polycethemia
49: Blood Bank in the Body is Spleen
50: Non Nucleated Blood cell is RBC
51: RBC produced in the Bone Marrow
52: River of Life is Called Blood
53: Normal Blood Cholesterol level 250mg/dl
54: Fluid part of Blood is Plasma
55: Normal Blood Sugar 100mg/dl

Jumatatu, 6 Agosti 2018

ENGLISH PSLE 2018

*ATTENTION CLASS SEVEN STAKE HOLDERS*

*_Standard seven pupils are close to their final examinations. I thought it is worth for teachers to remember a few important things._*

_*The examination format has changed. Today let's have a view on the English language new examination format*_

*Section A:  Grammar*
This section will consist of thirty (30) questions out of which ten (10) questions will be set from the topic of Tenses and 20 questions from other forms of grammar.
4.5.1.2 Candidates will be required to answer all the questions by choosing the correct answer from the given alternatives A, B, C, D and E. 

*Section B: Vocabulary*
This section will consist of six (6) multiple choice questions and will test the use of vocabulary in different context. 

Candidates will be required to answer all the questions by choosing the correct answer from the given alternatives A, B, C, D and E. 

*Section C: Composition*
This section will comprise of four (4) mixed/jumbled sentences. The candidate will be required to arrange the sentences logically so as to make a good composition.  

The sentences will be arranged using letters A to D.

*Section D: Comprehension*
This section will consist of a short passage which
will be followed by five (5) short answer questions.

Candidates will be required to read the passage and answer all the questions the space provided.
 
*Topics to be Examined*

1 Tenses 
2 Other forms of Grammar
3 Vocabulary 
4 Composition
5 Comprehension

My dear colleagues, let us prepare our children towards this current format. See you tomorrow for Social Studies Format

Tchao!
Moses Kyando
Educational Consultant
PPF House 6th Floor
Samora Avenue/Morogoro Road 0714414282

AINA ZA MANENO

AINA ZA MANENO

1. NOMINO Ni aina ya neno ambalo hutaja mtu, kitu, mahali, hali na kitendo. Mfano; Mwajuma, Kalamu, Mwanza, Udakitari, Kulima n.k.

Aina za nomino: • Nomino za pekee: Nomino za pekee hutaja na kutambulisha nomino mahsusi na za kipekee. Yaani kuwa kitu ni hicho na wala si chengine chochote. Hizi ni nomino zinazohusisha majina kama vile ya watu, nchi, miji, mito, milima, maziwa na bahari. Herufi za kwanza za nomono za pekee huwa kubwa hata kama nomino hizi zinapatikana katikati ya sentensi. Mfano; baba, Asha, Tanzania, Dodoma, Kilimanjaro, Victoria n.k

• Nomino za jamii: Hizi kwa jina jengine huitwa nomino za jumla. Nomino hizi hazibainishi wazi wazi vitu ambavyo habari zake zinatolewa. Kwa mfano ikiwa ni mtu, mahsusi hatambuliwi. Haituambii kama ni Kelvin, Tuafu ama Zawadi.Ikiwa ni ziwa halitambuliwi kama ni Michigan , Victoria au Nyasa, yaani hutaja vitu bila kutaja umahsusi wake kama ilivyo katika nomino za pekee. Hizi zinapoandikwa si lazima zianze kwa herufi kubwa isipokuwa zimetumiwa mwanzoni mwa sentensi au zimetumika kama anuani ya kutajia kitu kama vile Mkuu wa Sheria. Katika mfano huu ‘sheria’ kwa kawaida ni nomino ya kawaida, lakini hapa inaanza kwa herufi kubwa kwani inataja anuwani ya kipekee. Mfano wa nomino za kawaida ni; Mwanafunzi, Mwalimu, Mnyama, Mtazamaji, Askari n.k

• Nomino za kawaida: Kundi hili la nomino hutumia kigezo cha uwezekano wa kuhesabika kuziainisha. Hapa tunatofautisha kati ya nomino zinazowakilisha vitu vinavyohesabika kwa upande mmoja, na vile visivyohesabika kwa upande mwengine. Nomino ya vitu vinavyohesabika vitanda, nyumba, vikombe vitabu kadahlika. Zile zisizohesabika hurejelea vitu ambavyo hutokea kwa wingi na haviwezi kugawika, kwa mfano maji, mate, makamasi, maziwa, moshi, mafuta. Aghlabu nomino hizo huwa sawa katika umoja na wingi.

• Nomino za kitenzi jina: Hizi ni nomino zinazohusu vitenzi . Huundwa kwa kuongezwa kiambishi {ku-} cha unominishaji kwenye mzizi wa kitenzi cha kitendo halisi ili kukifanya kiwe nomino. Mfano; Kulima, Kucheza, Kuimba n.k

• Nomino dhahania: Hizi ni nomino ambazo hurejelea vitu vinavyoweza kuhusika na mwanaadamu kupitia milango ya hisia kama macho, mapua, masikio vidole na ulimi- yaani vitu ambavyo haviwezi kushikika, kuonekana, na kuonjeka. Mfano; Vita, Njaa, Ugonjwa, Shetani, Mungu n.k

2. VIVUMISHI • Ni maneno ambayo hutoa ufafanuzi au maelezo ya ziada kuhusu jina ili kuitambulisha vyema.

Aina za vivumishi.

• Vivumishi vya sifa: hutoa sifa za nomino /kiwakilishi cha nomino. Sifa hizi huweza kuwa nzuri, mbaya au yoyote ile. Mfano; mzuri, mbaya, mrembo n.k • Vivumishi vya idadi: vinaweza kujitokeza katika aina tatu ndogondogo. Vivumishi vya aina hii hutoa taarifa kuhusu idadi ya nomino ambazo kiwango chake kimetajwa. Mfano; wawili, watano, wengi, wachache n.k• • Vivumishi vya kumiliki: Ni vivumishi vinavyoonesha kuwa kitu fulani kina milikiwa na mtu au kitu chengine. Mfano; yangu, yake, yako, kwetu n.k • Vivumishi Vioneshi: Vivumishi vya aina hii huonyesha mahali au upande kitu kilipo. Vivumishi vya aina hii hujengwa na mzizi {h} kwa vitu vilivyopo karibu na mzizi {le} kwa vitu vilivyo mbali. Mfano; hapa, pale n.k • Vivumishi vya kuuliza: Hivi ni vivumishi ambavyo hufafanua nomino kwa kuuliza habari zake. Hujibu swali “gani? ipi? ngapi?” • Vivumishi vya pekee: Vivumishi hivi huitwa vya pekee kwa sababu kila kimojawapo huwa na maana maalumu. Pia kila kimojawapo huchukua upatanisho wake wa kisarufi kulingana na ngeli ya nomino ambayo kinaivumisha. Mizizi vivumishi hivi ni ote, o-ote, enye, -enyewe, - ingine, -ingineo. –ote. Huonyesha ujumla wa kitu au vitu -o-ote Kivumishi cha aina hii kina maana ya “kila”, “bila kubagua” – enye Kivumishi cha aina hii hutumika kuleta dhanna ya umilikishaji nomino Fulani. – enyewe Kivumishi cha aina hii hutumika kuisisitiza nomino fulani. – ingine Kivumishi cha aina hii huonyesha/huonesha ‘tofauti na’ au ‘zaidi ya’ kitu Fulani. – ingineo Kivumishi cha aina hii hutumika kuonesha/kuonyesha ziadi. • Vivumishi vya A- unganifu: Vivumishi vya aina hii huundwa kwa mzizi wa kihusishi a- unganifu. Kihusishi hiki huandamana na nomino kuunda kirai husishi ambacho huvumisha nomino iliyotajwa awali. Vivumishi vya aina hii hutumika kuleta dhanna zifuatazo:- -Umilikaji -Nafasi katika orodha. Mfano; wa kwangu, wa Juma, ya tano ya Sita n.k

4. VIELEZI Maana ya vielezi: Vielezi ni maneno yanayofafanua vitenzi, vivumishi au vielezi vyengine. Huweza kuarifu kitendo kilichotendeka kilitendeka wapi , namna gani na hata mara ngapi?

Aina za vielezi • Vielezi vya namna au jinsi. Vielezi vya namna hii huonyesha jinsi au namna kitendo kilivyotendeka. Vielezi vya namna vipo vya aina kadhaa. - Vielezi vya namna halisi. Hivi ni vielezi vinavyotumia maneno ambayo kimsingi yana sura ya vielezi moja kwa moja katika uainishaji wa aina za maneno. Mfano; kuimba sana -Vielezi vya namna mfanano Hivi ni vielezi ambavyo hutumika kufananisha vitendo na vivumishi au nomino mbalimbali. Hujengwa kwa kuongeza kiambishi (ki-) au kiambishi (vi-). Viambishi hivi hujulikana kwa jina la viambishi vya mfanano. Ulifanya vizuri kumsaidia mwanangu.

-Vielezi vya namna vikariri Hivi ni vielezi ambavyo hufafanua vitenzi kwa kurudiarudia neno moja mara mbili. Mfano; polepole, harakaharaka. - Vielezi vya namna hali Hivi ni vielezi ambavyo hufafanua juu ya kitendo kilichotendeka kimetendeka katika hali gani. Mfano; kivivu, kibabe, kizembe, kipole n.k - Vielezi vya namna ala/kitumizi Hivi ni vielezi vinavyotaja vitu ambavyo hutumika kutendea kitendo. Mfano; kwa kisu, kwa kalamu n.k - Vielezi vya namna viigizi. Hivi vinaelezea zaidi jinsi tendo lilivyofanyika kwa kuigiza au kufuatisha sauti inayojitokeza wakati tendo linapofanyika au kutokea. Mfano; alimpiga paaaah! • Vielezi vya idadi. Vielezi vya namna hii huonyesha kuwa kitendo kilitendeka mara fulani au kwa kiasi fulani. Mfano; amempiga mara mbili • Vielezi vya mahali.. Vielezi vya namna hii huonyesha mahali ambapo kitendo kinatokea.Huweza kudokezwa kwa viambishi au kwa maneno kamili. Mfano; amekaa jikoni • Vielezi vya wakati: Vielezi vya namna hii huonyesha wakati wa kutendeka kwa kitendo.Huweza kutokea kama maneno kamili au hodokezwa kwa kiambishi {po.} Mfano; alimkaribisha alipokuja.

5. VITENZI Kitenzi ni neno linaloeleza jambo lililotendwa au lililotendeka. Kitenzi huarifu lililofanyika au lililofanywa na kiumbe hai chochote kinachoweza kutenda jambo. Kitenzi cha Kiswahili huundwa na mzizi pamoja na viambishi vyenye uamilifu wa aina tofauti.

AINA ZA VITENZI • Vitenzi vikuu (T): Vitenzi vikuu ni vile ambavyo hubeba ujumbe muhimu wa kiarifu cha sentensi. Mfano; Mtoto amekuja.

• Vitenzi visaidizi: Hivi hutoa taarifa ya kusaidia vitenzi vikuu. Hutoa taarifa kama vile uwezekano , wakati, hali n.k.Vitenzi visaidizi daima hutumika na vitenzi vikuu, ndivyo vinavyobeba viambishi vya wakati. Mfano; Alikua anacheza, Huwa namfurahia. Vitenzi visaidizi huweza kupachikwa urejeshi wa nomino na kusaidia kuifafanua nomino hiyo. Mfano; motto aliyekua anacheza. Virejeshi hivyo ni kama; -ye-, -yo-, -o-, -lo-, -cho-, -wo- n.k

• Vitenzi vishirikishi: Hivi ni Vitenzi ambavyo hufanya kazi ya kuunga sehemu mbili za sentensi. Havichukui viambishi vya nafsi, njeo ama hali. Vitenzi vishirikishi ni vya aina mbili, ambavyo ni kitenzi kishirikishi “ni” cha uyakinishi na kitenzi shirikishi “si” cha ukanushi. Kazi za kitenzi kishirikishi -kushirikisha vipashio vingine katika sentensi -Kuonesha tabia fulani iliyopo au isiyokuwepo ya mtu fulani au kitu fulani. -Kuonyesha cheo au kazi anayofanya mtu. -kuonyesha sifa za mtu. - kuonyesha umoja wa vitu au watu -kuonyesha mahali -kuonyesha umilikishi wa kitu chochote. 6. KIWAKILISHI Kiwakilishi ni aina ya neno linaloweza kutumika badala ya jina .

AINA ZA VIWAKILISHI • Viwakilishi vya kuuliza/viwakilishi viulizi ambavyo huashiriwa na mofu / kiambishi {-pi} ambavyo katika tungo hutanguliwa na kiambishi ngeli cha jina husika. Mfano- Mtoto yupi • Wiwakilishi vya urejeshi ambavyo vinajengwa na shina amba pamoja na vipande vidogo vidogo –ye-, -o-, -cho-, vyo, lo, po, mo, ko n.k ambavyo vinachaguliwa kilingana na ngeli ya majina yanayorejeshwa navyo. • Viwakilishi vya idadi: Viwakilishi hivi hutuarifu kuhusu idadi ya nomino hiyo huweza kuwa kamili (halisi) au ya jumla. Mfano; Wengi wamekuja • Viwakilishi vya pekee:- Hivi ni aina ya vivumishi vya pekee kuwakilisha nomino. Hufuata sheria za upatanisho za nomino zinazowakilishwa. • Viwakilishi vya A-unganifu:- Viwakilishi hivi huundwa kwa kihisishi cha A-unganifu kusimamia nomino iliyomilkiwa, inayochukuwa nafasi fulani katika orodha au nomino ya aina fulani. Kihisishi a-unganifu huandamana na nomino kuunda kirai husishi ambacho husimama mahali pa nomino.

7. VIUNGANISHI Ni maneno, kikundi cha maneno au kiambishi chenye kuunganisha maneno, kirai, kishazi au sentensi.Dhima ya kiunganishi ni kuunga vipashio viwili au zaidi vyenye hadhi sawa kisarufi.

Aina za viunganishi: • Viunganishi huru: hivi ni viunganishi vinavyosimama pekee katika tungo, katikati ya vipashio vinavyo ungwa. Hujumuisha: - -Viunganishi nyongeza/vya kuongeza. Mfano; Tena, Na, Zaidi ya n.k. - Viunganishi vya sababu/visababishi. Mfano; Kwa kuwa, kwa sababu kwa vile, kutokana na, n.k. - Viunganishi linganishi/vya kinyume. Mfano; Ingawa, Japokuwa, Lakini n.k. - Viunganishi vya wakati. Mfano; kasha, baadaye, Halafu, Baada ya n.k. - Viunganishi vya masharti. Mfano; Kama, Ikiwa, Iwapo n.k - Viunganishi vihusishi Mfano; Cha, La, Wa, Za n.k.

• Viunganishi tegemezi: Ni viambishi ambavyo hutiwa katika kitenzi cha kishazi tegemezi ili kukiunga na kitenzi kikuu cha kishazi huru ambavyo kwa pamoja huunda sentensi changamano au shurtia. Mfano; -ye-, -po-, -ki-, -cho- na -nge-.

8. VIHUSISHI Ni maneno ambayo huonyesha uhusiano uliopo baina ya neno moja na jengine. Vihusishi aghlabu huonyesha uhusiano kati ya nomino au kirai nomino na maneno mengine. Mambo mbalimbali yanayoweza kuonyeshwa na vihusishi - huonyesha uhusiano wa kiwakati - huonyesha uhusiano wa mahali - huonyesha uhusiano wa kulinganisha - huonyesha uhusiano wa umilikaji - huonyesha uhusiano wa sababu/kiini

Aina za vihusishi

-vihusishi vya wakati Mfano; kabla ya, baada ya n.k -vihusishi vya mahali Mfano; chini ya, juu ya, ndani ya, mbele ya n.k. - vihusishi vya ulinganishi/ vya kulinganisha Mfano; kuliko, zaidi ya n.k. -vihusishi vya sababu/ kusudi/nia Mfano; kwa sababu ya, kwa ajili ya n.k. -vihusishi vya ala (kifaa)- Mfano; kwa - vihusishi vimilikishi Mfano; cha, za n.k. -vihusishi vya namna/jinsi/hali Mfano; moto wa kuotea mbali, macho ya mviringo Matumizi ya ziada ya kihusishi “kwa” -kihusishi hiki huonyesha mahali au upande -kihusishi hiki huonyesha sababu au kisababishi cha jambo -kihusishi hiki huonyesha wakati -kihusishi hiki huonyesha sehemu Fulani ya kitu kikubwa -kihusishi hiki hutumika kuonyesha ‘nia ya pamoja na’ -Kihusishi hiki huonyesha jinsi kitendo kilivyotendeka

9. VIHISISHI / VIINGIZI Ni maneno ambayo hudokeza hisia za moyoni mwa mzungumzaji baada ya kuwa katika hali ya furaha, huzuni, majonzi, maumivu, kushangaa, majuto n.k. Mara tunapotumia viingizi katika tungo huathiri tungo hiyo kuifanya kuwa na mshangao, hivyo tunaongeza alama ya mshangao mbele ya tungo hiyo. Kwa kuzingatia hisia tunaweza kuwa na aina ya viingizi zifuatazo:- • Viingizi vya huzuni – pole! Jamani! Maskini! N.k • Viingizi vya mshangao – waow! Lahaula! Eboo! Haiii! Ati! • Viingizi vya kuitika – abee! Lamaa! Naam! • Viingizi vya kutakia heri – Inshallah! • Viingizi vya kiapo – Wallah! Haki ya nani! Kweli kabisa!

Jumapili, 5 Agosti 2018

KARUDI BABA MMOJA

1. Karudi baba mmoja,
toka safari ya mbali,
Kavimba yote mapaja,
na kutetemeka mwili,
Watoto wake wakaja,
ili kumtaka hali,
Wakataka na kauli iwafae maishani.

2. Akatamka mgonjwa,
ninaumwa kwelikweli,
Hata kama nikichanjwa,
haitoki homa kali,
Roho naona yachinjwa,
kifo kimenikabili,
Semeni niseme nini,
kiwafae maishani.

3. Yakawatoka kinywani,
maneno yenye akili,
Baba yetu wa thamani,
sisi tunataka mali,
Urithi tunatamani,
mali yetu ya halali,
Sema iko wapi mali,
itufae maishani

4. Baba aliye kufani,
akajibu lile swali,
Ninakufa maskini,
baba yenu sina hali,
Neno moja lishikeni,
kama mnataka mali,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.

5. Wakazidi kumchimba,
baba mwenye homa kali,
Baba yetu watufumba,
hatujui fumbo hili,
akili zetu nyembamba,
hazijajua methali,
Kama tunataka mali,
tutapataje shambani?

6. Kwanza shirikianeni,
nawapa hiyo kauli,
Fanyeni kazi shambani,
mwisho mtapata mali,
haya sasa buriani,
kifo kimeniwasili,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.

7. Alipokwisha kutaja,
fumbo hili la akili,
Mauti nayo yakaja,
roho ikaacha mwili,
Na watoto kwa umoja,
wakakumbuka kauli,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.

8. Fumbo wakatafakari,
watoto wale wawili,
wakakata na shauri,
baada ya siku mbili,
wote wakawa tayari,
pori nene kukabili,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.

9. Wakazipanda shambani,
mbegu nyingi mbalimbali,
tangu zile za mibuni,
hadi zitupazo wali,
na mvua ikaja chini,
wakaona na dalili,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.

10. Shamba wakapalilia,
bila kupata ajali,
Mavuno yakawajia,
wakafaidi ugali,
Wote wakashangilia,
wakakumbuka kauli,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.

11. Wakanunua na ng'ombe,
majike kwa mafahali,
wakapata na vikombe,
mashine na baiskeli,
Hawakuitaka pombe,
sababu pombe si mali,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.

12. Wakaongeza mazao,
na nyumba za matofali,
Pale penye shamba lao,
wakaihubiri mali,
Wakakiweka kibao,
wakaandika kauli...

"KAMA MNATAKA MALI
MTAIPATA SHAMBANI".
🚶🚶🚶🚶🚶🚶

Miaka hiyo tuliimba tu kama kujifurahisha wala hatukujua maana yake, leo twatambua nini maana yake

Nawakumbusha tu
🏃🏾

Jumanne, 31 Julai 2018

KWANINI HUOLEWI??

KWA NINI WANAWAKE WENGI SIKU HIZI HAWAOLEWI? WENGI HUPISHANA NA WAUME ZAO

Kwamfano
- Mwanamke anapigiwa simu kwa namba ngeni, anauliza namba yangu umeitoa wapi? Usiponiambia aliyekupa usinipigie. HAPO UMEPISHANA NA MUME

- Mwanamke anaingia ndani ya daladala, amekaa na mwanaume, kwa maringo, anachukua earphone na kuweka masikioni na kuwasha mziki ili asiongeleshwe. HAPO UMEPISHANA NA MUME.

- Mwanamke anasalimiwa njiani, anaitikia, akiongeleshwa tena anachuna. HAPO UMEPISHANA NA MUME.

- Mwanamke unatumiwa meseji inbox, hujibu. HAPO UMEPISHANA NA MUME.

- Mwanamke unapigiwa simu na mwanaume, unaona kabisa anakupigia ila hutaki kupokea tu. HAPO UMEPISHANA NA MUME.

- Mwanamke unakwenda gheto kwa mwanaume, una mkoba wako, ukifika muda wa kuondoka unaomba nauli. HAPO UMEPISHANA NA MUME.

- Mwanamke unakwenda kwa mwanaume, badala ya kusonga ugali, cha kwanza unataka chipsi kuku. HAPO UMEPISHANA NA MUME.

- Mwanamke unaanza uhusiano na mwanaume, siku ya pili tu unamwambia bebi sina hela ya vocha. HAPO UMEPISHANA NA MWANAUME.

- Mwanamke upo na mwanaume, anakwambia agiza chochote, bila kujishtukia unaagiza bia. HAPO UMEPISHANA NA MUME.

- Mwanamke unachati na mwanaume, chatting zako ni K, P, Pw.
HAPO UMEPISHANA NA MUME.

- Mwanamke unaweka picha mapaja wazi, kifua umebust. HAPO UMEPISHANA NA MUME.

- Mwanamke unamwambia mwanaume akutumie video za ngono kwenye simu. HAPO UMEPISHANA NA MUME.

Usilalamike kwamba kwa nini mpaka sasa hivi hujaolewa. Niambie sasa ni mara ngapi umepishana na mume!

Jumatatu, 30 Julai 2018

UJASILIAMALI

Fursa 150 za Biashara na Miradi Mbalimbali Nchini Tanzania

MUUNGWANA BLOG / 


1. Kununua Mashine za kukoroga zege na kukodisha.
2. Kununua Mashine za kukata vyuma na kuzikodisha.
3. Kutengeneza na kuuza tofali
4. Ufundi, Website updating/Database: Katika Halmashauri, Manispaa, Mashule, Wizara, Wilaya na           Makampuni mbalimbali.
5.  Kuanzisha kituo cha redio na televisheni
6. Kufunga na kutengeneza vifaa mbalimbali vya electroniki na mawasiliano mfano; compyuta na vifaa       vya compyuta na mawasiliano.
7. Kuuza software; mfano Antivirus, Operating Systems, Pastel, Tally, Myob, n.k
8. Kushona na kuuza nguo.
9. Kufungua Duka la kuuza nguo mpya; suit, socks, batiki, nguo za asili, Mashuka, Mashati, Suruali,
10. Ufugaji wa mifugo mbalimbali mfano Kondoo, Mbuzi, Ng’ombe, Kuku, Bata, na wengine.
11. Kufungua stationery, kuuza (supply) vitabu na vifaa mbalimbali ktk mashule na vyuo.
12. Kutoa ushauri mbalimbali wa Kitaalamu.
13. Kuuza viazi, mahindi, mihogo, kutengeneza popcorn na kuziuza.
14. Kusajili namba za simu na kuuza vocha
15. Kuwa na mradi wa Pikipiki zisizotumia mafuta na zinazotumia mafuta
16. Kilimo cha mazao mbalimbali kulingana na hali ya hewa ya sehemu husika.
17. Kuuza Mitumba
18. Kusimamia miradi mbalimbali
19. Kufungua duka la kuuza mitambo mbalimbali
20. Kufungua banda la chakula na chips
21. Kukodisha turubai viti na meza
22. Kufungua Supermarket
23. Kufungua Saluni
24. Kufungua Bucha
25. Video Shooting & Editing.
26. Kufungua Internet cafe
27. Duka la kuuza matunda
28. Kufungua duka la kuuza vifaa vya simu za mkononi na landline.
29. Kufungua duka la vifaa vya ujenzi; cement, vifaa vya umeme, duka la mabati
30. Kutengeneza michoro mbalimbali ya majumba na miradi ya ICT
31. Kuchapa vitabu, bronchures, n.k
32. Kuanzisha kampuni ya ujenzi (Building contractor)
33. Kuuza Vifaa vya umeme wa nishati ya jua (solar) ,battery, inverter na vifaa vingine vya solar n.k
34. Kuuza maji kwa jumla na rejaleja.
35. Kutengeneza na kuuza Unga wa lishe bora.
36. Kukodisha Music
37. Kuanzisha Mradi wa Taxi
38. Kuanzisha mradi wa Daladala
39. Kuuza vifaa vya Kompyuta, laptops, converters, HDDs, Monitors, Softwares, CD Copiers na vifaa           vingine.
40. Kununua magenerator na kukodisha
41. Kufungua kampuni ya kutoa huduma za simu
42. Kufungua kampuni ya kutoa huduma za internet (ISP)
43. Kuuza mabati na vigae
44. Kujenga apartments
45. Kufungua Kisima cha mafuta ya taa au mafuta ya aina zote
46. Kufungua Duka la samaki
47. Kufungua Duka la nafaka
48. Kufungua Shule za Awali, Shule za Msingi, Sekondari na Vyuo.
49. Kujenga hostel
50. Kuuza vocha na ving’amuzi vya DStv, Zuku, Startimes, Easy TV, TNG, Digitech, Continental.
51. Kujenga mtambo wa kuzalisha umeme na kuuza katika viwanda na wananchi.
52. Ufundi simu
53. Kufungua Hospitali, Zahanati.
54. Maabara ya Macho, Meno
55. Kuchimba/Kuuza Madini
56. Kufungua ofisi ya kutoa huduma ya simu na fax
57. Kuuza miti na mbao
58. Kufungua Grocery, bar
59. Kufungua studio ya kupiga na kusafisha picha
60. Kucharge simu/battery
61. Duka la TV na vifaa vingine
62. Kuanzisha biashara ya kuuza vyakula katika sherehe na tamasha mbalimbali (catering).
63. Banda la kupigisha simu
64. Kuuza na kushona Uniform za shule
65. Kuanzisha duka la kuuza vitu kwa jumla.
66. Kufungua gereji za kutengeneza bajaji, pikipiki na magari
67. Kuuza vyuma, pembejeo, rake, jembe
68. Kuuza fanicha
69. Kufungua sehemu ya kuziba pancha za matairi
       ya magari na mitambo.
70. Kujenga nyumba za kulala wageni (hotel)
71. Kuagiza na kuuza vifaa vya aluminium.
72. Kuuza vioo
73. Kushona na kukodisha nguo za harusi
74. Kufungua yard kwa ajili ya kuosha magari
75. Kuuza mashine za kuchomelea (welding machine).
76. Kuuza vifaa vya kuvaa Site (boots, helmets etc)
77. Kununua mabasi kwa ajili ya kusafirisha wanafunzi
78. Kufungua studio ya kutengeneza vipindi vya redio na televisheni
79. Kuanzisha ofisi ya michezo ya televisheni (TV Games)
80. Kufungua benki
81. Kuwa na malori ya kubeba kokoto na mchanga
82. Kuuza vifaa mfano TV, CCTV Camera, n.k
83. Kuwa dalali wa vitu mbalimbali
84. Kuanzisha mradi wa kukodisha fork lift na winchi (crane)
85. Kuanzisha kiwanda cha kutengeneza viatu.
86. Kuanzisha viwanda mbalimbali
87. Duka la vifaa vya simu na gadgets mbalimbali zinazoendana na mawasiliano ya Vodacom, TTCL,          AIRTEL, TIGO, ZANTEL, n.k.
88. Kujenga Ukumbi wa kukodisha kwa sherehe, mikutano mbalimbali
89. Kununua matrekta, mitambo ya ujenzi wa barabara na kukodisha
90. Kutengeneza antenna na kuuza
91. Kufungua mradi wa Machine za kusafisha, kutoboa na kuchana mbao
92. Kufungua mradi wa kuuza vifaa vya Umeme wa kutumia upepo
93. Biashara ya kuagiza magari
94. Kufanya biashara za Jukebox
95. Kukodisha matenki ya maji
96. Kufungua duka la kuuza Asali
97. Kutengeneza Mikokoteni/ matoroli na kuikodisha
98. Kufungua Duka la vinyago, batiki
99. Kuanzisha huduma ya AIRTEL MONEY, MPESA, TIGOPESA, EZY PESA
100. Kuanzisha sehemu ya kufanyia mazoezi (Gym).
101. Kununua na kuuza vifaa vya kupima ardhi.
102. Kufungua duka la kuuza dawa (pharmacy).
103. Kufungua Kampuni ya Ulinzi
104. Kufungua kampuni ya "Clearing and fowarding"
105. Kuchezesha vikaragosi
106. Kuuza spea za bajaji, magari na pikipiki
107. Kuuza baiskeli
108. Kuuza magodoro
109. Kuuza vyombo mbalimbali kwa ajili ya matumizi ya nyumbani mfano bakuli, sahani, vikombe,                 vijiko,
110. Kuuza marumaru (limestones)
111. Kuuza kokoto
112. Kuuza mchanga
113. Kufundisha Tuisheni
114. Biashara za bima
115. Kampuni ya kusafirisha abiria kwa njia ya anga (ndege)
116. Biashara za kitalii
117. Biashara za meli na maboti.
118. Kampuni ya kuchimba visima
119. Kufungua ofisi ya wakili/mawakili wa kujitegemea
120. Kuuza mkaa
121. Kutengeneza mashine za kutengeneza tofali
122. Kampuni ya kupima ardhi
123. Kampuni ya magazeti
124. Kuchapa (printing) magazeti
125. Kuuza magazeti
126. Kuchimba mafuta
127. Kiwanda cha kutengeneza mabati
128. Kiwanda cha kutengeneza fanicha
129. Kiwanda cha kutengeneza matairi
130. Kutengeneza vitanda vya chuma
131. Kununua nyumba katika Maghorofa (Apartments) na kuzikodisha.
132. Kukodisha makapeti
133. Kupamba maharusi na kumbi za harusi/sherehe.
134. Mashine ya kusaga na kukoboa nafaka.
135. Kazi ya ususi na kusafisha kucha.
136. Kuuza Gypsum
137. Malori ya kubeba mafuta na Mizigo
138. Duka la kuuza mboga za majani
139. Duka la kuuza maua.
140. Kampuni ya kuzoa takataka
141. Kampuni ya kuuza magari
142. Kuuza viwanja
143. Uvuvi
144. Kutengeneza na kuuza nguzo za kujengea fensi
145. Uchoraji wa mabango.
146. Duka la kuuza silaha
147. Ukumbi wa kuonesha mpira
148. Biashara ya mlm (network marketing)
149. Yadi kwa ajili ya kupaki magari
150. Mradi wa trekta za kukodisha kwa ajili ya kilimo

Ijumaa, 27 Julai 2018

MUONEKANO MPYA WA MTIHANI KISWAHILI DARASA LA SABA

*WANAFUNZI WETU WANAPOKARIBIA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA NI VIZURI WALIMU TUJIKUMBUSHE YAFUATAYO*

_*Mfumo mpya wa kutahini darasa la saba umebadilika, maswali sasa ni 45. Kila somo limetolewa ufafanuzi juu ya maeneo ya upimaji tamati na namna ya upimaji tamati huo utakavyokuwa. Leo tuanze na KISWAHILI*_

*Sehemu A: Sarufi* 
Sehemu hii itakuwa na maswali ishirini (20) ya kuchagua Maswali yatajikita katika kubainisha aina za maneno, kutumia kwa usahihi aina mbalimbali za maneno, miundo ya sentensi na nyakati mbalimbali.

Mtahiniwa atatakiwa kujibu maswali yote katika sehemu hii kwa kuchagua jibu sahihi kutoka katika chaguzi A, B, C, D na E.
 
*Sehemu B: Lugha ya Kifasihi*
Sehemu hii itakuwa na maswali kumi (10) ya kuchagua.  Mtahiniwa atatakiwa kujibu maswali yote.

Maswali katika sehemu hii yatakuwa ya kuchagua jibu sahihi kutoka katika chaguzi A, B, C, D na E.

Maswali  yatajikita katika mada ya methali, nahau na vitendawili.

*Sehemu C: Ushairi*
Sehemu hii itakuwa na maswali sita (6) ya kuchagua jibu lililo sahihi. Mtahiniwa atatakiwa kujibu maswali yote.

Maswali katika katika sehemu hii yatakuwa ya kuchagua jibu sahihi kutoka katika chaguzi A, B, C, D na E.

Maswali hayo hayo yatajikita zaidi katika mada ya ushairi na tenzi

*Sehemu D: Utungaji/Uandishi wa Habari na Barua*
Sehemu hii itakuwa na sentensi nne (4) zilizochanganywa ambapo mtahinwa atatakiwa kuzipanga katika mtiririko unaoleta maana.

Maswali haya yatakuwa ya kuchagua sentensi sahihi kutoka katika chaguzi A, B, C na D.

Mtahiniwa atatakiwa kujibu maswali yote.

*Sehemu E: Ufahamu*
Sehemu hii itakuwa na maswali matano (5) na mtahiniwa atatakiwa kujibu maswali yote.

Maswali yote yatakuwa ya kujaza nafasi iliyoachwa wazi.

Maswali yatajikita katika ufahamu wa kusoma habari.


*Mada Zitakazotahiniwa*

1 Sarufi 
2 Lugha ya kifasihi 
3 Ushairi 
4 Utungaji/Uandishi wa Barua/Uandishi wa Habari 
5 Ufahamu

Kesho tutapitishana kwenye somo jingine. Lengo hapa ni kuwakumbusha walimu kutunga mitihani hasa hii ya kujiandaa kwa kuzingatia mwongozo.

Ahsanteni sana
Moses Kyando
Mshauri wa Elimu
PPF House 6th Floor
0714414282

JIFUNZE KISWAHILI

*TUJIFUNZE KISWAHILI MAANA KINAKUA KWA KASI;*

*1. Charger - Kimemeshi.*

*2. Remote - Kitenzambali.*

*3. Password - Nywila.*

*4. Akala (bladder shoes) - Kirikiri.*

*5. Passion Fruit - Karakara.*

*6. Kangaroo - Bukunyika.*

*7. Fridge - Jokofu.*

*8. Juice - Sharubati.*

*9. Chips - Vibanzi.*

*10. PHD - Uzamifu.*

*11. Masters Degree - Uzamili.*

*12. Degree - Shahada.*

*13. Diploma - Stashahada.*

*14. Certificate - Astashahada.*

*15. Keyboard - Kicharazio.*

*16. Scanner - Mdaki.*

*17. Flash disk - Diski Mweko.*

*18. Mouse (for a computer) - Kiteuzi.*

*19. Floppy Disk - Diski Tepetevu.*

*20. Computer virus - Mtaliga.*

*21. Distillation - Ukenekaji.*

*22. Evaporation - Mvukizo.*

*23. Synthesis - Uoanishaji.*

*24. Oesophagus - Umio.*

*25. Greenhouse - Kivungulio.*

*26. Femur - Fupaja.*

*27. Germ cell - Selizazi.*

*28. Humus - Mboji.*

*29. Nector - Mbochi/Ntwe.*

*30. Nutrients - Virutubisho.*

*31. Crystal - Fuwele.*

*32. Appetizers - Vihamuzi.*

*33. ATM - Kiotomotela.*

*34. Business Card - Kadikazi.*

*35. Scratch Card - Kadi Hela.*

*36. Simcard - Kadiwia/Mkamimo.*

*37. Memory Card - Kadi Sakima.*

*38. Microwave - Tanuri Ya Miale.*

*39. Mobile Phone - Rununu/Rukono.*

*40. Stapler - Kibanizi.*

*41. Laptop - Kipakatalishi.*

*42. Power Saw - Msumeno Oto.*

*43. Duplicating Machine - Kirudufu.*

*44. Photocopier - Kinukuzi.*

*45. Cocktail Party - Tafrija Mchapulo.*

*46. Air Conditioner - Kiyoyozi.*

*47. Calculator - Kikokotozi.*

*48. Lift - Kambarau.*

*49. Reaction - Radiamali.*

*50. Toothpick - Kimbaka.*

*#Share*

Jumatano, 25 Julai 2018

METHALI MBALIMBALI

METHALI MIA SITA NA KUMI (610)
1. Aanguaye huanguliwa.
2. Asiye sikia la mkuu, huvunjika guu.
3. Abebwaye hujikaza.
4. Adhabu ya kaburi aijuae maiti.
5. Adui aangukapo, mnyanyue.
6. Adui mpende.
7. Adui wa mtu ni mtu.
8. Afadhali ya Musa kuliko ya Firauna.
9. Ahadi ni deni.
10. Ajidhaniaye amesimama, aangalie asianguke.
11. Akiba haiozi.
12. Akili ni mali.
13. Akili ni nywele kila mtu ana zake.
14. Akili nyingi huondowa maarifa.
15. Akutukanae hakuchagulii tusi.
16. Akipenda chongo huita kengeza.
17. Akufaae kwa dhiki, ndiye rafiki.
18. Akufanyiaye ubaya, mlipe wema.
19. Akupaye kisogo si mwenzio.
20. Akutendaye mtende, mche asiyekutenda.
21. Alisifuye jua, limeuangaza.
22. Aliye juu msubiri chini.
23. Aliye kando, haangukiwi na mti.
24. Aliye kupa wewe kiti (kibao) ndiye aliye nipa mimi kumbi.
25. Aliye kutwika, ndiye atakaye kutua.
26. Akufukuzae hakwambii toka.
27. Aliyekupa mkeka ndiye aliyenipa kumbesa.
28. Amani haipatikani mpaka kwa ncha ya upanga.
29. Ana hasira za mkizi.
30. Anayekuja pasi na hodi, huondoka bila ya kuaga.
31. Angurumapo simba, mcheza ni nani?
32. Aninyimaye mbazi kanipunguzia mashuzi.
33. Apewaye ndiye aongezwaye.
34. Anaejipiga mwenyewe, halii.
35. Asifuye mvuwa imemnyea.
36. Asiye kubali kushindwa si mshindani.
37. Asiye kujua, hakuthamini.
38. Asiye kuwapo na lake halipo.
39. Asiye lelewa na mamae hulelewa na ulimwengu.
40. Asiye na mengi, ana machache.
41. Asiye uliza, hanalo ajifunzalo.
42. Asiyejua maana, haambiwi maana.
43. Atangaye na jua hujuwa.
44. Atangazaye mirimo, si mwana wa ruwari (Liwali).
45. Atekaye maji mtoni hatukani mamba.
46. Avumaye baharini papa kumbe wengi wapo.
47. Baada ya dhiki faraja.
48. Bahari hailindwi.
49. Bamba na waume ni bamba, hakuna bamba la mume.
50. Bandu bandu huisha gogo.
51. Baniani mbaya, kiatu chake dawa.
52. Bendera hufuata upepo.
53. Biashara asubuhi.
54. Bilisi wa mtu ni mtu.
55. Bora kinga kuliko tiba.
56. Bora lawama kuliko fedheha.
57. Bora mchawi kuliko fitina.
58. Biashara asubuhi.
59. Bora nusu shari kuliko shari kamili.
60. Bwawa limeingia ruba.
61. Cha mtu mavi.
62. Chaka la samba, halilali nguruwe.
63. Chamlevi huliwa na mgema.
64. Chanda chema huvikwa pete.
65. Chelewa chelewa, utakuta mtoto si wako.
66. Choko mchokoe pweza, binaadamu hutomuweza.
67. Chombo cha kuzama hakina usukani.
68. Chovya - chovya yamaliza buyu la asali.
69. Chui hakumbatiwi.
70. Chururu si ndo ndo ndo.
71. Dalili ya mvua mawingu.
72. Damu nzito kuliko maji.
73. Daraja livuke ulifikapo.
74. Dawa ya moto ni moto.
75. Daraja ukilibomoa, ujue kuogelea.
76. Dau la mnyonge haliendi joshi, likienda joshi ni matakwa ya Mungu.
77. Dawa ya moto ni moto.
78. Donda ndugu halina dawa.
79. Dua ya kuku haimpati mwewe.
80. Fadhila huna, hata hisani hukumbuki?
81. Fadhila ya nyuki ni moto.
82. Fadhila ya punda ni mateke (mashuz)
83. Fahari ya macho haifilisi duka.
84. Farasi hamuwawezi, tembo mtawalishani?
85. Fata nyuki ule asali.
86. Fimbo ya mbali haiui nyoka.
87. Fumbo mfumbe mjinga, mwerevu huligangua.
88. Funika kombe mwanakharamu apite.
89. Ganda la mua la jana, chungu kaona kivuno.
90. Gome la udi, si la mnuka uvundo.
91. Haba na haba, hujaza kibaba.
92. Haki ya mtu hailiki.
93. Hakuna masika yaso mbu.
94. Hakuna msiba usio na mwenziwe.
95. Hakuna siri ya watu wawili.
96. Hakuna ziada mbovu.
97. Hala hala mti na macho.
98. Hamadi ni ilio kibindoni, na silaha ni iliyo mkononi.
99. Hapana marefu yasio na mwisho.
100. Haraka haraka haina baraka.
101. haraka haraka haina baraka.
102. Haramu yako halali kwa mwenzio.
103. Hasidi hasada.
104. Hasidi mbaya.
105. Hasira, hasara.
106. Hatua ndefu hufupisha mwendo.
107. Hauchi hauchi, unakucha.
108. Hayawi hayawi, mara huwa.
109. Heri kufa macho kuliko kufa moyo.
110. Heri kujikwa kidole kuliko ulimi.
111. Heri nitakula na nini?, kuliko nitakula nini?
112. Heri ya marama kuliko kuzama.
113. Hiari ya shinda utumwa.
114. Hogo halihogoki mpaka kwa hogo jenziwe.
115. Hucheka kovu asiye kuwa na jeraha.
116. Ila ya kikwapa, kunuka pasipo kidonda.
117. Yaliyoopita si ndwele, ganga yajayo.
118. Iliyo jaa ndiyo ipunguzwayo.
119. Imara ya jembe kaingojee shambani.
120. Jambo usilolijua, usiku wa giza.
121. Jina jema hungara gizani.
122. Jini likujualo halikuli likakwisha.
123. Jino la pembe si dawa ya pengo.
124. Jitihada haiondoi kudura.
125. Jitihadi haiondoi kudura.
126. Jogoo la shamba haliwiki mjini.
127. Jungu kuu, halikosi ukoko.
128. Jununu fununu.
129. Kafiri akufaaye, si muislamu asiye kufaa
130. Kafiri akufaye si Isilamu asiyekufa.
131. Kama hujui kufa,tazama kaburi.
132. Kama wewe wasema cha nini, mwezio asema nitakipata lini.
133. Kamba hukatika pabovu.
134. Kanga hazai ugenini.
135. Kawaida ni kama sheria.
136. Kawia ufike.
137. Kazi mbaya siyo mchezo mwema.
138. Kelele za chura hazimzuwii ng'ombe kunywa maji.
139. Kelele za mlango haziniwasi usingizi (Kelele za mlango hazimuudhi mwenye nyumba)
140. Kenda karibu na kumi.
141. Kesho kesho, kesho kiama.
142. Kiburi si maungwana.
143. Kibuzi na kibuzi hununua jahazi.
144. Kichango kuchangizana.
145. Kidole kimoja hakivunji chawa.
146. Kikulacho ki nguoni mwako.
147. Kikushindacho kukila usikitie ila.
148. Kila chombo kwa wimblile.
149. Kila mbwa hubwekea mlangoni kwao.
150. Kila mlango na ufunguwo wake.
151. Kila mtoto na koja lake.
152. Kila mtu huzikwa na kaburi lake.
153. Kila mtu na bahati yake.
154. Kila mwamba ngoma ,ngozi huivuta kwake.
155. Kila mtu hulilia mamae.
156. Kila ndege huruka kwa ubawa wake.
157. Kila shetani na mbuyu wake.
158. Kilimia kikizama kwa jua, huzuka kwa mvua, na kikizama kwa mvua, huzuka kwa jua.
159. Kilio huanza mfiwa ndipo wa mbali wakaingia.
160. Kimya kingi kina mshindo mkubwa.
161. Kinga na kinga ndipo moto uwakapo.
162. Kingiacho mjini si haramu.
163. Kinyozi hajinyoi.
164. Kinywa ni jumba la maneno.
165. Kipendacho moyo dawa.
166. Kipofu hasahau mkongojo wake.
167. Kipya kinyemi ingawa kidonda.
168. Kisebusebu na kiroho papo.
169. Kisokula mlimwengu, sera nale.
170. Kisokula mlimwengu,sera nale.
171. Kisu kimenifika mfupani.
172. Kitanda usicho kilalia hukijui kunguni wake.
173. Kitumbua kimeingia mchanga.
174. Kivuli cha fimbo hakimfichi mtu jua.
175. Kiwi cha yule ni chema cha; hata ulimwengu uwishe.
176. Kizuri chajiuza kibaya chajitembeza.
177. Konzi ya maji, haifumbatiki.
178. Konzo ya maji haifumbatiki.
179. Kosa moja haliachi mke.
180. Kozi mwandada, kulala na njaa kupenda.
181. Kuagiza kufyekeza.
182. Kuambizana kuko kusikilizana hapana.
183. Kucha M'ngu si kilemba cheupe.
184. Kuchamba kwingi, kuondoka na mavi.
185. Kufa kufaana.
186. Kufa kwa jamaa, harusi.
187. Kufa kwa mdomo,mate hutawanyika.
188. Kufanaya kosa sio kosa, kosa ni kurudia kosa.
189. Kuishi kwingi, kuona mengi.
190. Kujikwa si kuanguka,bali ni kwenda mbele.
191. Kujikwaa si kuanguka, bali ni kwenda mbele.
192. Kukopa harusi kulipa matanga.
193. Kukopa harusi, kulipa matanga.
194. Kuku havunji yai lake.
195. Kuku mgeni hakosi kamba mguuni.
196. Kula kutamu ,kulima mavune.
197. Kulea mimba si kazi kazi kulea mwana.
198. Kukopa harusi, kulipa matanga.
199. Kumuashia taa kipofu ni kuharibu mafuta.
200. Kunako matanga kume kufa mtu.
201. Kunguru mwoga hukimbiza mbawa zake.
202. Kupanda mchongoma, kushuka ndio ngoma.
203. Kupata si werevu, na kukosa si ujinga.
204. Kupoteya njia ndiyo kujua njia.
205. Kurambaramba ndio kula, kunenepa kwake Mola.
206. Kusikia si kuona.
207. Kutangulia si kufika.
208. Kutoa ni moyo usambe ni utajiri.
209. Kutu kuu ni la mgeni.
210. Kuugua sio kufa.
211. Kuvuja kwa pakacha nafuu ya mchukuzi.
212. Kuzima koleo si mwisho wa uhunzi.
213. Kwa mwoga huenda kicheko na kwa shujaa huenda kilio.
214. Kweli ilio chungu, si uongo ulio mtamu.
215. Kwenda mbio siyo kufika.
216. Kwenye miti hakuna wajenzi.
217. La kuvunda halina rubani.
218. La kuvunda halina ubani.
219. Lake mtu halimtapishi bali humchefua.
220. Leo kwako, kesho kwa mwenzio.
221. Leo ni leo asemayo kesho ni mwongo.
222. Liandikwalo ndiyo liwalo.
223. Lila na fila hazitangamani.
224. Lipitalo, hupishwa .
225. Lisemwalo lipo,ikiwa halipo laja.
226. Lisilo na mkoma, hujikoma lilo.
227. Lisilokuwapo moyoni, halipo machoni.
228. Maafuu hapatilizwi.
229. Macho hayana pazia.
230. Mafahali wawili hawakai zizi moja.
231. Maiti haulizwi sanda.
232. Maji hayapandi mlima.
233. Maji hufuata mkondo.
234. Maji ukiyavuliya nguo huna budi kuyaoga.
235. Maji usiyoyafika hujui wingi wake.
236. Maji ya kifuu, bahari ya chungu.
237. Maji yakijaa hupwa.
238. Maji yakimwagika hayazoleki.
239. Maji yamenifika shingoni.
240. Majuto ni mjukuu.
241. Mali ya bahili huliwa na wadudu.
242. Mama ni mama, hata kama ni rikwama.
243. Mama nipe radhi kuishi na watu kazi.
244. Mambo kunga.
245. Manahodha wengi chombo huenda mrama.
246. Maneno makali hayavunji mfupa.
247. Maneno mazuri humtowa nyoka pangoni.
248. Maneno si mkuki.
249. Mapenzi ni kikohozi, hayawezi kufichika.
250. Masikini akipata matako hulia mbwata.
251. Masikini haokoti,akiokota huambiwa kaiba.
252. Masikini na mwanawe tajiri na mali yake.
253. Maskini hana kinyongo.
254. Mavi usioyala, wayawingiani kuku?
255. Mavi ya kale hayanuki.
256. Mbinu hufuata mwendo.
257. Mbio za sakafuni huishia ukingoni.
258. Mbiu ya mgambo ikilia kuna jambo.
259. Mchagua jembe si mkulima.
260. Mchagua nazi hupata koroma.
261. Mchagua nazi si mfuaji.
262. Mchakacho ujao,halulengwi na jiwe.
263. Mchama ago hanyeli,huenda akauya papo.
264. Mchamba kwingi mara ujitia dole.
265. Mcheka kilema hafi bila kumpata.
266. Mchele mmoja mapishi mengi.
267. Mchelea mwana kulia hulia yeye..
268. Mcheza hawi kiwete, ngoma yataka matao.
269. Mcheza kwao hutuzwa.
270. Mcheza na tope humrukia.
271. Mchezea mavi, hayaachi kumnuka.
272. Mchezea zuri, baya humfika.
273. Mchimba kisima hungia mwenyewe.
274. Mchonga mwiko hukimbiza mkono wake.
275. Mchuma janga hula na wakwao.
276. Mchumia juani,hulia kivulini.
277. Mdharau biu, hubiuka yeye.
278. Mdharau mwiba humchoma.
279. Meno ya mbwa hayaumani.
280. Mfa maji haachi kutapatapa.
281. Mfa maji hukamata maji.
282. Mficha uchi hazai.
283. Mfinyazi hulia gaeni.
284. Mfuata nyuki hakosi asali.
285. Mfukuzwa kwao hana pakwenda.
286. Mgaagaa na upwa hali ugari kande.
287. Mganga hajigangi.
288. Mgema akisifiwa tembo hulitia maji.
289. Mgeni ni kuku mweupe.
290. Mgeni njoo mwenyeji apone.
291. Mgomba haushindwi na mkunguwe.
292. Mgonjwa haulizwi uji.
293. Miye nyumba ya udongo, sihimili vishindo.
294. Mjinga akierevuka mwerevu yupo mashakani.
295. Mjinga mpe kilemba utamuona mwendowe.
296. Mjumbe hauawi.
297. Mkaidi hafaidi mpaka siku ya idi.
298. Mkamatwa na ngozi ndiye mwizi.
299. Mkamia maji hayanywi.
300. Mkamia maji hayanywi.
301. Mkataa la mkuu huvunjika guu.
302. Mkataa wengi ni mchawi.
303. Mkataa ya Musa hupata ya Firauna.
304. Mke ni nguo, mgomba kupalilia.
305. Mkono moja hauchinji ng'ombe.
306. Mkono moja haulei mwana.
307. Mkono mtupu haulambwi.
308. Mkono usioweza kuukata,ubusu.
309. Mkosa kitoweo humangiria.
310. Mkuki kwa nguruwe, kwa mwanadamu uchungu.
311. Mkulima ni mmoja walaji ni wengi.
312. Mla cha mwenziwe na chake huliwa.
313. Mla cha uchungu na tamu hakosi.
314. Mla kuku wa mwenziwe miguu humwelekea.
315. Mla mbuzi hulipa ngombe.
316. Mla mla leo mla jana kala nini?
317. Mla nawe hafi nawe ila mzaliwa nawe.
318. Mlala na maiti haachi kulia lia.
319. Mlenga jiwe kundini hajui limpataye.
320. Mlimbua nchi ni mwananchi.
321. Mnyamaa kadumbu.
322. Mnywa maji kwa mkono mmoja,Kiu yake i pale pale.
323. Moja shika, si kumi nenda urudi.
324. Moto hauzai moto.
325. Mpanda farasi wawili hupasuka msamba.
326. Mpanda ngazi hushuka.
327. Mpanda ovyo hula ovyo.
328. Mpemba akipata gogo hanyii chini.
329. Mpemba hakimbii mvua ndogo.
330. Mpende akupendae asiyekupenda achana naye.
331. Mpiga ngumi ukuta huumiza mkonowe.
332. Mpofuka ukongweni,hapotewi na njia.
333. Msafiri kafiri.
334. Msafiri masikini ajapokuwa sultani.
335. Msasi haogopi mwiba.
336. Msema kweli hukimbiwa na rafiki zake.
337. Msema pweke hakosi.
338. Mshika kisu, hashiki makalini.
339. Mshale kwenda msituni haukupotea.
340. Mshoni hachagui nguo.
341. Msi bahati, habahatishi.
342. Msi mbele, hana nyuma.
343. Msishukuru mja, hamshukuru Molawe.
344. Msitukane wagema na ulevi ungalipo.
345. Msitukane wakunga na uzazi ungalipo.
346. Mstahimilivu hula mbivu.
347. Mtaka cha mvunguni sharti ainame.
348. Mtaka lake hasindwi.
349. Mtaka nyingi nasaba hupata mwingi msiba.
350. Mtaka unda haneni.
351. Mtaka uzuri hudhurika.
352. Mtaka yote hukosa yote.
353. Mtegemea nundu haachi kunona.
354. mtegemea nundu, haachi konona.
355. Mtego bila ya chambo, haunasi.
356. Mtembezi hula miguu yake.
357. Mteuzi heshi tamaa.
358. Mti hauwendi ila kwa nyenzo.
359. Mtondoo haufi maji.
360. Mtoto akililia wembe mpe.
361. Mtoto umleyavyo ndivyo akuavyo.
362. Mtoto wa nyoka ni nyoka.
363. Mtu hakatai mwito,hukata aitwalo.
364. Mtu hujikuna ajipatapo.
365. Mtu huulizwa amevaani ,haulizwi amekulani.
366. Mtumai cha ndugu hufa masikini.
367. Mtumi wa kunga haambiwi maana.
368. Mtumikie kafiri upate mradi wako.
369. Mtupa jongoo hutupa na mti wake.
370. Muhitaji khanithi walau kana rijaali.
371. Muiba yai leo kesho hua mwizi wa ng'ombe.
372. Mume wa mama ni baba.
373. Mungu hamfichi mnafiki.
374. Mungu si asumani.
375. Muonja asali haonji mara moja.
376. Muuza sanda, mauti kwake harusi.
377. Mvua nguo, huchutama.
378. Mvumbika changa hula mbovu.
379. Mvumbika pevu hula mbivu na mvumbika changa hula mbovu.
380. Mvungu mkeka.
381. Mvunja nchi ni mwananchi.
382. Mvuvi ajuwa pweza alipo.
383. Mwacha asili ni mtumwa.
384. Mwamba na wako hukutuma umwambiye.
385. Mwamini Mungu si mtovu.
386. Mwana maji wa kwale kufa maji mazowea.
387. Mwana mkuwa nawe ni mwenzio kama wewe.
388. Mwana simba ni simba.The child of lion is a lion.
389. Mwana wa kuku hafunzwi kuchakura.
390. Mwana wa mtu ni kizushi, akizuka, zuka naye.
391. Mwanga mpe mtoto kulea.
392. Mwangaza mbili moja humponyoka.
393. Mwanzo kokochi mwisho nazi.
394. Mwanzo wa chanzo ni chane mbili.
395. Mwanzo wa ngoma ni lele.
396. Mwapiza la nje hupata la ndani.
397. Mwekaji kisasi haambiwi mwerevu.
398. Mwenda bure si mkaa bure,huenda akaokota.
399. Mwenda mbio hujikwa kidole.
400. Mwenda omo na tezi marejeo ni ngamani.
401. Mwenda pole hajikwai.
402. Mwenda wazimu hapewi panga.
403. Mwenda wazimu hapoi, bali hupata nafuu.
404. Mwenye haja hwenda chooni.
405. Mwenye kelele hana neno.
406. Mwenye kovu usidhani kapowa.
407. Mwenye kubebwa hujikaza.
408. Mwenye kuchinja hachelei kuchuna.
409. Mwenye kuumwa na nyoka akiona jani hushtuka.
410. Mwenye macho haambiwi tazama.
411. Mwenye mdomo hapotei.
412. Mwenye nguvu mpishe.
413. Mwenye njaa hana miko.
414. Mwenye pupa hadiriki kula tamu.
415. Mwenye shibe hamjui mwenye njaa.
416. Mwenye shoka hakosi kuni.
417. Mwenye tumbo ni tumbole, angafunga mkaja.
418. Mwenzako akinyolewa wewe tia maji.
419. Mwibaji na watwana, mlifi ni mwungwana.
420. Mwili wa mwenzio ni kando ya mwilio.
421. Mwizi hushikwa na mwizi mwenziwe.
422. Mwomba chumvi huombea chunguche.
423. Mwosha hadhuru maiti.
424. Mwosha huoshwa.
425. Mwosha husitiri maiti.
426. Mzaha,mzaha, mara hutumbuka usaha.
427. Mzazi haachi ujusi.
428. Mzigo usiouweza unaubebea nini?
429. Mzigo Wa mwenzio ni kanda Ia usufi.
430. Mzika pembe ndiye mzua pembe.
431. Mzowea kutwaa, kutoa ni vita.
432. Mzowea vya kunyonga, vya kuchinja haviwezi.
433. Mzungu Wa kula hafundishwi mwana.
434. Nahodha wengi, chombo huenda mrama.
435. Nani kama mama?
436. Natuone ndipo twambe, kusikia Si kuona.
437. Nazi haishindani na jiwe.
438. Nazi mbovu harabu ya nzima.
439. Ndege mjanja hunaswa na tundu bovu.
440. Ndege mwigo hana mazowea.
441. Ndevu sio shani, hata beberu anazo.
442. Ndugu chungu, jirani mkungu.
443. Ndugu mwui afadhali kuwa naye.
444. Ndugu wakigombana, chukua jembe ukalime, wakipatana chukua kikapu ukavune.
445. Ngoja! ngoja? huumiza matumbo.
446. Ngoma ivumayo haidumu.
447. Ngoma ivumayo haikawii kupasuka.
448. Ngoma ya kitoto, haikeshi.
449. Ng'ombe avunjikapo guu hurejea zizini.
450. Ng'ombe haelemewi na nunduye.
451. Ngombe wa Maskini hazai.
452. Ngozi ivute ili maji. ( Udongo upate uli maji )
453. Nguo ya kuazima, Haistiri matako.
454. Nia njema ni tabibu, nia mbaya huharibu.
455. Nifae na mvua nikufae na jua.
456. Nimekula asali udogoni, utamu ungali gegoni.
457. Nimekupaka wanja, wewe wanipaka pilipili.
458. Nimerejesha kikombe na kisahani chake.
459. Njia ya muongo fupi.
460. Njia ya mwongo ni fupi.
461. Njia ya siku zote haina alama.
462. Nta Si asali; nalikuwa nazo Si uchunga.
463. Nyani haoni kundule, huliona la mwenziwe.
464. Nyani haoni kundule.
465. Nyimbo mbaya haibembelezewi mtoto.
466. Nyimbo ya kufunzwa haikeshi ngoma.
467. Nyongeza huenda kwenye chungu.
468. Nyota njema huonekana asubuhi.
469. Nyumba usiyolala ndani huijui ila yake.
470. Nyumba ya udongo haihimili vishindo.
471. Nzi kufa juu ya kidonda Si haramu. (Jihadi ya nzi, kufa kidondani)
472. Ondoa dari uwezeke paa.
473. Pabaya pako Si pema pa mwenzako.
474. Padogo pako Si pakubwa pa mwenzako.
475. Painamapo ndipo painukapo.
476. Paka akiondoka, panya hutawala.
477. Paka hakubali kulala chali.
478. Paka hashibi kwa wali, matilabaye ni panya.
479. Paka wa nyumba haingwa.
480. Panapo wengi hapaharibiki neno.
481. Papo kwa papo kamba hukata jiwe.
482. Pele hupewa msi kucha.
483. Pema usijapo pema; ukipema Si pema tena.
484. Penye kuku wengi usimwage mtama.
485. Penye mafundi, hapakosi wanafunzi.
486. Penye mbaya wako, hapakosi mwema wako/na mwema wako hakosi.
487. Penye miti hakuna wajenzi.
488. Penye nia pana njia.
489. Penye urembo ndipo penye urimbo.
490. Penye wazee haliharibiki neno.
491. Penye wengi pana mengi.
492. Penye wengi pana Mungu.
493. Pilipili usoila, wewe inakuwashia nini?
494. Pole pole ndio mwendo.
495. Pwagu hupata pwaguzi.
496. Radhi ni bora kuliko mali .
497. Radhi za wazee, ni fimbo.
498. Sahani iliyofunikwa, kilichomo kimesitirika.
499. Sahau ni dawa ya Waja.
500. Samaki mmoja akioza, huoza wote.
501. Samaki mpinde angali mbichi.
502. Shida haina hodi.
503. Shida huzaa maarifa.
504. Shika! Shika! na mwenyewe uwe nyuma.
505. Shimo Ia ulimi mkono haufutiki.
506. Shoka lisilo mpini halichanji kuni.
507. Si kila king'aacho ni dhahabu.
508. Si kila mwenye makucha huwa simba.
509. Si Mungu mtupu na mkono wa mtu.
510. Sikio halilali na njaa.
511. Sikio halipwani kichwa. (Sikio halipiti kichwa).
512. Sikio Ia kufa halisikii dawa.
513. Siri ya mtungi aijuaye ni kata.
514. Sitaacha kula mkate kwa kuogopa kiungulia.
515. Siku njema huonekana asubuhi.
516. Siku utakayokwenda uchi, ndiyo siku utakayokutana na mkweo.
517. Siku ya kufa nyani, miti yote huteleza.
518. Siku za mwizi, arubaini.
519. Simba mwenda kimya (pole) ndiye mla nyama.
520. Simbiko haisimbuki ila kwa msukosuko.
521. Sio shehe bali ni shehena.
522. Siri ya maiti aijuaye muosha.
523. Sitafuga ndwele na waganga tele.
524. Sitapiki nyongo harudi haramba.
525. Subira ni ufunguo Wa faraja.
526. Sumu mpe paka, mbuzi utamdhulumu.
527. Sumu ya neno ni neno.
528. Tabia ni ngozi ya mwili.
529. Tamaa mbele, mauti nyuma.
530. Taratibu ndio mwendo.
531. Tawi kavu kuanguka si ajabu.
532. Teke Ia kuku halimuumizi mwanawe
533. Tonga si tuwi
534. Tunda jema halikawii mtini.
535. Ucheshi wa mtoto ni anga Ia nyumba.
536. Ujuzi hauzeeki.
537. Uchungu wa mwana, aujue mzazi.
538. Udongo uwahi ungali maji (Udongo upate uli maji)
539. Udugu wa nazi hukutania chunguni (Udugu wa nazi hukutana pakachani)
540. Uji hajauonja, tayari ushamuunguza
541. Ukenda kwa wenye chongo, fumba lako jicho.
542. Ukimpa shubiri huchukua pima.
543. Ukimuiga tembo kunya, utapasuka Makalio.
544. Ukimwamsha alolala utalala weye.
545. Ukinyofoa mnofu, ukumbuke kuguguna mfupa.
546. Ukiona kwako kunaungua kwa mwenzako kunateketea.
547. Ukiona moshi, chini kuna moto.
548. Ukiona neno, usiposema neno, hutapatikana na neno.
549. Ukiona vinaelea, vimeundwa.
550. Ukiona zinduna, na ambari iko nyuma.
551. Ukistahi mke ndugu, huzai nae.
552. Ukitaja nyoka, shika fimbo mkononi.
553. Ukitaka kula nguruwe, chagua aliye nona.
554. Ukitaka salama ya dunia, zuia ulimi wako.
555. Ukiujua wa mbele, nina ujua wa nyuma.
556. Ukupigao ndio ukufunzao.
557. Ukuukuu wa kamba Si upya wa ukambaa.
558. Ulimi hauna mfupa.
559. Ulimi unauma kuliko meno.
560. Ulipendalo hupati, hupata ujaaliwalo.
561. Ulivyoligema, utalinywa.
562. Umeadimika kama la jogoo.
563. Umegeuka mung'unye waharibika ukubwani.
564. Umejigeuza pweza, unajipalia makaa?
565. Umekuwa bata akili kwa watoto?
566. Umekuwa nguva, huhimili kishindo?
567. Umeruka mkojo unakanyaga mavi.
568. Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu.
569. Unajenga kwa mwenzio na kwako kunaporomoka!!
570. Unakuja juu kama moto wa kifuu.
571. Unamlaumu mwewe, kipanga yuwesha kuku.
572. Ungalijua alacho nyuki, usingalionja asali.
573. Ushikwapo shikamana (Ukibebwa usijiachie).
574. Usiache kunanua kwa kutega.
575. Usiache mbachao kwa msala upitao.
576. Usiache tawi kabla ya kushika tawi.
577. Usiandikie mate na wino ungalipo
578. Usicheze na simba, ukamtia mkono kinywani.
579. Usijifanye kuku mweupe.
580. Usikaange mbuyu ukawaachia wenye meno
581. Usile na kipofu ukamgusa rnkono.
582. Usimgombe mkwezi, nazi imeliwa na mwezi.
583. Usiniache njia panda.
584. Usinikumbushe kilio matangani.
585. Usinipake mafuta kwa nyuma ya chupa.
586. Usinivishe kilemba cha ukoka.
587. Usione simba kapigwa na mvua.
588. Usipoziba ufa utajenga ukuta.
589. Usisafirie nyota ya mwenzio.
590. Usisahau ubaharia kwa sababu ya unahodha.
591. Usishindane na Kari; Kari ni mja wa Mungu.
592. Usitukane wagema na ulevi ungalipo.
593. Usitukane wakunga na uzazi 'ungalipo.
594. Utakosa mtoto na maji ya moto.
595. Usiyavuke maji usiyoweza kuyaoga.
596. Utaula na chua kwa uvivu wa kuchagua.
597. Vita havina macho.
598. Vita si lele mama.
599. Vita vya panzi, neema ya kunguru
600. Waarabu wa pemba, hujuana kwa vilemba
601. Wache waseme.
602. Wafadhilaka wapundaka.
603. Wagombanao ndio wapatanao.
604. Watu wanahisabu nazi, wewe unahisabu makoroma.
605. Wapiganapo tembo wawili ziumiazo ni nyasi.
606. Watetea ndizi, mgomba si wao.
607. Wazuri haweshi.
608. Wema hauozi..
609. wengi wape.
610. Zinguo la mtukufu, ni ufito.

Alhamisi, 14 Juni 2018

WORLD CUP FIXTURE

For all football ⚽ lovers

*FIFA WORLD CUP 2018(RUSSIA) FIXTURES WITH INDIAN TIMING. There will be 64 matches in TOTAL*

*Group A:-* Russia, Saudi Arabia, Egypt, Uruguay 
*Group B:-* Portugal, Spain, Morocco, Iran 
*Group C:-* France, Australia, Peru, Denmark 
*Group D:-* Argentina, Iceland, Croatia, Nigeria 
*Group E:-* Brazil, Switzerland, Costa Rica, Serbia 
*Group F:-* Germany, Mexico, Sweden, South Korea 
*Group G:-* Belgium, Panama, Tunisia, England 
*Group H:-* Poland, Senegal, Colombia, Japan

*THURSDAY, June 14/6/2018*
1.RUSSIA vs SAUDI ARABIA  (8:30pm)

*FRIDAY, June 15/6/2018*
2.EGYPT vs URUGUAY (5:30pm)
3.Morocco vs Iran (8:30pm)
4.Portugal vs Spain (11:30pm)

*SATURDAY, June 16/6/2018*
5.FRANCE vs AUSTRALIA (3:30pm)
6.ARGENTINA vs ICELAND  (6:30pm)
7.PERU vs DENMARK (9:30pm)
8.CROATIA vs NIGERIA (5:30pm)

*SUNDAY, June 17/6/2018*
9.COSTA RICA vs SERBIA (12:30am)
10.GERMANY vs MEXICO (8:30pm)
11.BRAZIL vs SWITZERLAND (11:30pm)

*MONDAY, June 18/6/2018*
12.SWEDEN vs SOUTH KOREA (5:30pm
13.BELGIUM vs PANAMA 8:30pm
14.TUNISIA vs ENGLAND 11:30pm

*TUESDAY, June 19/6/2018*
15.POLAND vs SENEGAL (5:30pm)
16.COLOMBIA vs JAPAN (8:30pm)
17.RUSSIA vs EGYPT (11:30pm)

*WEDNESDAY, June 20/6/2018*
18.PORTUGAL vs MOROCCO (5:30pm)
19.URUGUAY vs SAUDI ARABIA (8:30pm)
20.IRAN vs SPAIN (11:30pm)

*THURSDAY, June 21/6/2018*
21.FRANCE vs PERU (5:30pm)
22.DENMARK vs AUSTRALIA (4:30pm)
23.ARGENTINA vs CROATIA (11:30pm)

*FRIDAY, June 22/6/2018*
24.BRAZIL vs COSTA RICA (5:30pm)
25.NIGERIA vs ICELAND (8:30pm)
26.SERBIA vs SWITZERLAND (4:30pm)

*SATURDAY, June 23/62018*
27.BELGIUM vs TUNISIA (5:30pm)
28.GERMANY vs SWEDEN (8:30pm)
29.SOUTH KOREA vs MEXICO (11:30pm)

*SUNDAY, June 24/6/2018*
30.ENGLAND vs PANAMA (5:30pm)
31.JAPAN vs SENEGAL (8:30pm)
32.POLAND vs COLOMBIA (11:30pm)

*MONDAY, June 25/6/2017*
33.SAUDI ARABIA vs EGYPT (7:30pm)
34.URUGUAY vs RUSSIA (8:30pm)
35.IRAN vs PORTUGAL (11:30pm)
36.SPAIN vs MOROCCO (10:30pm)

*TUESDAY, June 26/6/2018*
37.AUSTRALIA vs PERU (7:30pm)
38.DENMARK vs FRANCE (7:30pm)
39.NIGERIA vs ARGENTINA (11:30pm)
40.ICELAND vs CROATIA (11:30pm)

*WEDNESDAY, June 27/6/2018*
41.S. KOREA vs GERMANY (7:30pm)
42.MEXICO vs SWEDEN (7:30pm)
43.SERBIA vs BRAZIL (11:30pm)
44.SWITZERLAND vs COSTA RICA (11:30pm)

*THURSDAY, June 28/6/2018*
45.JAPAN vs POLAND (7:30pm)
46.SENEGAL vs COLOMBIA (7:30pm)
47.PANAMA vs TUNISIA (11:30pm)
48.ENGLAND vs BELGIUM (10:30pm)

*LAST -16:-*
*SATURDAY, June 30/6/2018*
49.Group C-1st vs D-2nd (7:30pm)
50.Group A-1st vs B-2nd (11:30pm)

*SUNDAY, July 1/7/2018*
51.Group B-1st vs A-2nd (7:30pm)
52.Group D-1st vs Group C-2nd (11:30pm)

*Monday, July 2/7/2018*
53.Group E-1st vs F-2nd (12:30am)
54.Group G-1st vs Group H-2nd (11:30pm)
55.Group F-1st vs E-2nd (7:30pm)
56.Group H-1st vs G-2nd (11:30pm)

*QUARTER-FINALS:-*
*Friday, July 6/7/2018*
57.Winner 49 vs winner 50 (7:30pm)
58.Winner 53 vs winner 54 (11:30pm)

*SATURDAY, July 7/7/2018*
59.Winner 55 vs winner 56 (11:30pm)
60.Winner 51 vs winner 52 (12:00am)

*SEMI-FINALS:-*
*TUESDAY, July 10/7/2018*
61.Winner 57 vs winner 58 (11:30pm)

*WEDNESDAY, July 11/7/2018*
62.Winner 59 vs winner 60 (11:30pm)

*THIRD-PLACE PLAY-OFF:-*
Saturday, July 14/7/2018
63.Loser 60 vs Loser 62

*FINAL:-*
Sunday, July 15/7/2018
64. Winner 61 vs winner 62 (8:30pm)

MANCHESTER UNITED 2018/2019

MECHI ZA UFUNGUZI ENGLAND

Jumatano, 13 Juni 2018

SOMO LINAENDELEA

DALILI KUU 6 ZINAZOONYESHA MTU AMBAYE ATACHELEWA SANA KUFANIKIWA.

1)Siku zote ana pesa za kununua vocha na kuweka vifurushi,ana pesa za kununua nguo  lakini hana pesa za kununua kitabu kitakachomuongezea maarifa.

2)Siku Zote ana muda wa kuchart watsapp, kuangalia Movie,kusoma magazeti na Kupiga stori za mpira ama za wasanii lakini hana muda wa Kusoma kuhusu taaluma yake ama mambo ya kumpongeza ujuzi.

3)Siku zote akiona waliofanikiwa anawatuhumu aidha wameiba, ni freemason ama wana bahati katika maisha.Huwachukia na hataki kujifunza Kwao.

4)Siku zote hupenda kuhalalisha kufeli kwake kwa kujitetea,kulaumu uchumi,wazazi,serikali au amerogwa.

5)Siku Zote Hujiona anajua Kuliko Mtu Yeyote Yule na hapendi Kujifunza kwa wengine. Huongea sana Kuliko Kusikiliza.

6)Kila anachoingiza anatumia,ukimwambia kusave ama kuwekeza anasema ngoja nipate cha ziada nitaanza kesho.

Je Unayo dalili mojawapo kati ya hizo?

SWALI LA MTOTO

“Baba kwani mtu akifa anaweza kumnunulia mtu zawadi?” Lilikua ni swali kutoka kwa mwanangu wa miaka 5, nilistuka kidogo kwani alikua anazungumzia mambo ya kufa. Ndiyo kwanza tulikua tumetoka kuzunguka Mlimani City kwaajili ya kuwanunulia wanangu watatu zawadi na tulikaa kidogo ili kunywa Juice kabla ya kurejea nyumbani. Nilimuuliza kwanini anasema hivyo lakini hakua tayari kunijibu, aliniambie nimjibu tu na kumuambia “Hapana, mtu akishakufa hawezi kufanya kitu chochote.”
Nilimuona alivyonyong’onyea na kila nilivyojaribu kumchangamsha hakuchangamka tena. Nilirudi nyumbani na kuanza kugombana na mke wangu nikimuambia ni kwanini wanangu wanazungumzia habari za kufa kipindi kile. Alisema hajui chochote lakini nilijua tu ni yeye tu kawajaza ujinga wanangu, nilikasirika sana na kila wakati niliwaambia wanangu wasiwaze chochote kwani Baba yao nipo na siendi popote.
Siku zilienda na sikukuu ilikua inakaribia, wanangu wote walikua na furaha kasoro Anna peke yake, yule ambaye aliniuliza kuhusu kufa, kila wakati nilipojaribu kumpa vizawadi na kumfurahisha alikua akiishia kulia tu. Sikujua anausmbuliwa na nini lakini nilihisi kuna kitu, mpaka wakati mwingine niliogopa na kudhani kua labda kwakua ni mtoto kuna kitu kaoteshwa na maisha yangu yapo hatarini lakini niliziondoa hizo fikra.
Usiku mmoja nikiwa nimetulia chumbani Anna alikuja chumbani, mkononi alikua amebeba begi lake la shule, alikuja na kukaa kitandani, alikua analia, niliacha kusoma Kitabu na kumkumbatia nikimuuliza tatizo ni nini, hakusema chochote zaidi ya kufungua Begi lake. Alitoa fungu la hela elfu mojamoja na miatano tano zilikua nyingi kidogo, bila kuzihesabu zilikua zinafika kama elfu hamsini hivi. Alinikabidhi zile hela, nilimuuliza kazipata wapi na kwanini ananipa ndipo akanijibu.
“Nizakwangu Baba, nimekua nikikusanya Poket Money unayonipa na zawadi ili nikupe ukamnunulie Dada Jane nguo mpya, yeye Baba yake amefariki hawezi kumnunulia zawadi kama unavyotununulia sisi hivyo anakua anavaa nguo mbaya kila sikukuu. Nataka umnunulie ili uwe kama Baba yake, mimi siwezi kumnunulia kwani mimi si mwanaume siwezi kuwa Baba yake, yeye hana Baba”
Nilikuta machoazi yanaanza kunidondoka kama mtoto mdogo. “Nimefanya nini?” Niliwaza. Jane ni mtoto wa kwanza wa mke wangu, alizaa na mwanaume mwingine kabla sijakutana naye na yule mwanaume kumtelekeza hivyo mke wangu alikua anamlea yeye mwenyewe. Ingawa hakumuambia hivyo lakini ni kama kila mtu alijua kuwa Baba yake Jane kafariki ndiyo maana alikua haji kumtembelea.
Baada ya kumuoa nilianza kuishi naye, ingawa mwanzo niliona itakua kawaida na nilikua nikimpenda Jane lakini baada ya mimi kupata watoto wangu niliwapenda zaidi, nilimtenga na kusema kweli sikumchukulia kama mwanangu, sikujua kama wanangu wanajua kwani muda wote nilikua nawapa kila kitu nawanunulia zawadi huku Jane nikimtenga. Mpaka pale Anna aliponipa ile hela ndiyo nilijua kua inawaumiza wanangu namna ninavyomtenga Jane.
Machozi yalinidondoka uchungu nilioupata ulinifanya nijione kama mnyama. “Hivi napata faida gani kumtenga mtoto wa watu asiye na hatia, huyu si Dada wa wanangu? Kwani ni shilingi ngapi kumpenda huyu Binti…” Niliwaza mambo mengi bila majibu, nilikua katika lindi la mawazo mpaka Anna aliponistua “Baba utamnunulia nguo Dada Jane?” Nilimuambia ndiyo na kumuambia abaki na zile pesa nitamnunulia na pesa zangu.
Siku iliyofuata niliwachukua wanangu wote na mke wangu na ilikua ni siku ya kumnunulia mke wangu pamoja na Jane zawadi. Mke wangu alishangaa upendo niliomuonyesha Jane siku ile, Jane mwenyewe lishangaa kwani nilikua mtu mpya sana, alikua na furaha mpaka machozi, kila wakati alikua na wasiwasi, hata kuchagua nguo aligopa aloposikia bei yake, hakujua nini kimetoke lakini nilimuaomba msamaha mke wangu na kumuambia Jane sasa nitakua Baba yake, sasa najiona mtu mwenye furaha zaidi.
%%%MWISHO

KAZI KWENU WABABA WENYE KUWATENGA WATOTO WA KAMBO NA KUWAJARI WAKWENU SIKUKUU HIYO
MUNGU AWAFANYIE WEPESI

mwalimubahati

Jumanne, 12 Juni 2018

UNGEFANYA NINI HAPA?

NAWATAKIA MJADALA MWEMA:
Mkeo Anarudi Nyumbani kavimba vibaya usoni! Unamuuliza anakujibu kuwa kakutana na vibaka wamemvamia na kumpiga, lakini ukimcheki kwa makini unakuta kila kitu chake amerudi nacho na kiko salama. Unaanza kupeleleza, unagundua kapigwa na “Mchepuko” wake. Unaoneshwa mchepuko huo, nawe unakwenda moja kwa moja (straight) kwa huyo jamaa, unapomuuliza anakujibu kama ifuatavyo:
".....Bro mimi yule ni Mpnz wangu wa muda mrefu hata kabla hujamuoa, tuna miaka mingi ni wapnz wa siku nyingi sana. Mimi nakujua wewe kuwa huyo ni mkeo, ulimuoa wakati mimi sina uwezo kifedha, lakini hatukuwahi kugombana, tumeendelea na mapnz Muda mrefu, na hata watoto unaodhani ni wako, Mimi mwenyewe tulipanga majira, sasa yawezekana nami yupo wangu, kwani huwa natoa matumizi ya mtoto mmoja yule Jenerose. So kuwa na amani, nakufahamu vema.
"....Lakini kilichoniuma sana mimi ni kwamba huyu Mwanamke mshnz, nimegundua ananichet mimi, anatembea na njemba fulani, so iliniuma sana, nilitamani sana ufahamu hili, lakini ningeanzaje kukwambia wakati wewe hujui kama mimi mkeo ni mpnz wangu. Mimi sina tatizo na wewe, na hata akiniambia jana mmefanya sijali, lakini kwanini atembee na mwanmum mwingine tofauti na sisi (wewe na mimi). Kwahiyo kweli nimemfumua hayo makonde, tena kajikanda hapa.
"....Amebadilika sana huyu mwanamke, amekuwa na tabia chafu sana siku hizi, haiwezekani nichangie na mwanamme mwingine kwa mtu ninayempenda. Wee mwenyewe hujui tu ninavyoumia………”
Swali
Kama ndo wewe, utafanyaje, utaanza na huyo jamaa au utarudi mdogo mdogo kwa mkeo? Je utamfanya nini Mkeo?