Jumanne, 25 Juni 2019

KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI YA MTAA

*KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI YA MTAA.*

Katika kuchagua viongozi wa ngazi ya Serikali ya Mtaa, tafuteni Watanzania wenye sifa zifuatazo:

(i) *Awe mchapakazi* mwenye kujitoa sadaka kuwatumikia watu, hasa wananchi wa kawaida;

(ii) *Awe mwepesi* kuona, kusikiliza na kuguswa na shida za wananchi wake. Tena awe jasiri katika kupigania haki za wanyonge na awe na uwezo na ubunifu katika kutatua kero za wananchi hao;

(iii) *Awe mwadilifu*, anayechukia na kupiga vita rushwa na ufisadi kwa matendo;

(iv) *Anayetambua fursa* zilizopo katika eneo lake, kubuni mikakati ya kuwaendeleza wananchi anaowaongoza na kuwatia watu wake hamasa ya kuthubutu kutumia fursa hizo;

(v) *Awe mtetezi hodari* wa kulinda mazingira na mpambanaji dhidi ya athari za mabadiliko ya tabianchi; 

(vi) *Mwenye kutoabudu nyadhifa*; anayetambua kuwa nafasi na vyeo tulivyopewa ni vya muda tu. Ni vya kupita! Thamani halisi ya kiongozi ni kufanya kazi kwa bidii na kuacha kumbukumbu nzuri kwa ustawi wa eneo analoliongoza na Taifa kwa ujumla; 

(vii) *Awe kama mchezaji mzuri* wa kiungo katika timu ya ushindi, anayetambua kwamba mkono mmoja hauwezi kupiga makofi ya shangwe;

(viii) *Awe mwenye kutambua kwamba kazi za kiongozi* zina maana sana kwa kuwa zinamwezesha kubadilisha maisha ya maelfu ya Watanzania, hasa wanyonge, kuwa bora zaidi;

(ix) *Awe na uwezo wa kuwaeleza wananchi kinaganaga* kuhusu Serikali yao inawapeleka wapi na wajibu wa kila mmoja ili waendelee kuiunga mkono; na

(x) *Awe anatoka ndani ya chama cha siasa(CCM)* kinachotetea maslahi na haki za wanyonge na chama hicho ni CCM!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni