Jumatano, 26 Juni 2019

MAMBO YANAYO HAMASISHA MAHABA KWA MUME.

MAMBO YANAYO HAMASISHA MAHABA KWA MUME.

1 *KITANDA*
_*Mwanamke jitahidi kitanda chako kiwe vizuri NA cha kuvutui kipambe vizuri, kwa mashuka mazuri yenye nakshi, na shuka inyooke vizuri, sio kitanda kinakuwa kama  vile stoo ya nguo chafu.*_

2. *MANUKATO*
_*Katika chumba chako jitahidi sana, kiwe kinanuka kila Mara mumeo anapo rudi akiingia chumbani akutane na harufu nzuri, sio chumba chanuka jasho.*_

3. *USAFI*
_*Hili ni jambo la muhimu sana maana  utakuta chumbani kuna vyupi vya wiki nzima, hazijafuliwa mataulo chini, masidiria, mumeo akikuta chumba kiko hivo ujue unaondoa mvuto.*_

4. *USAFI WA MWILI.*
_*Pia usafi wa mwili, mwanaume anavutiwa na utakavokuwa umejipamba na atavutiwa kimapenzi na wewe sio vichaka, au mwiko unatoka na kutu, mwili anakutana na chumvichumvi kwenye ulimi wake sio sahihi jamani.*_

5. *KUJIPAMBA.*
_*Mke jipambe vile mume anapenda sio ulazimishe mapambo yako mfano piko huwa inawamaliza ipake au hina kachore viua, wanja, shanga, bangili, kipini, kikuku, marashi, UDI, na kusuka vile anapenda sio kutwa kushinda na janaba.*_

6. *MAPOKEZI MAZURI.*
_*Wanaume wanapenda sana kupokelewa vizuri, kwa mahaba tele mapokezi utakayo mpa mtu jitahidi yawe ya mahaba, legeza macho, mwili, yaani ili mradi tu umchanganye mwanaume, Siyo umeshupaa kma mwanajeshi kwenye paredi.*_

7. *CHAKULA*
_*Jitahidi mwanamke kujua kupika sio tu kupika michakula kama ya jela michukuchuku mibaya, mamchuzi chururu kama watoto wanapika.*_

8. *MITEGO*
_*Hii ni njia ambayo  watakiwa uwe mjanja ukimuona mumeo kakaa sebleni basi vaa hata shumizi jipitishe huku ukijitingisha Mara kwa Mara,ujue lazima atakutizama tu tena kwa mwendo nzuri wa maringo.*_

9. *MAPENZI*
_*Mapenzi si lazima kitandani tu popote  ni muhimu maana wengine mpaka  mume amwambie cheza basi.*_

10. *UKARIMU NA  KUJIPENDEKEZA KAULI TAMU.*
_*Hata kama kwenu ulizoea kuwa na domo kama bakuli la togwa jitahidi kuchunga mdomo ukiona huwezi mumeo ngoja aondoke ufunge mlango ubwatuke peke yako kaa chizi, akirudi funga upuuzi wako zungumza maneno mazuri mnyenyekee.*_

11. *MAKELELE*
_*Wanaume wengi huwa hawapendi makelele wanapenda wakirudi nyumbani kuwe kumetulia isiwe kma  choo cha umma, Wanaume wanapenda ukimya mahala panapokuwa kimya huzidisha mapenzi, sauti toa  kitandani mukifanya  tendonii na sio mida mingine.*_

12. *ZAWADI*
_*Jitahidi kumnunulia vizawadi  pindi unapokwenda sokoni au dukani mwanaume hujisikia faraja pale ukimpatia zawadi sio akupe wewe tu hata pipi.*_

13. *MAVAZI*
_*Pendelea kumchagulia mavazi tazama rangi ya mwili wake kisha mchagulie nguo inayoendana na rangi yake ya mwili  siyo mume mweusi waende kumvisha nguo nyekundu  kma anaenda kupunga mapepo  mamaa.!!!*

Mlale unono.... Mimi Bibi Sabry

Jumanne, 25 Juni 2019

KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI YA MTAA

*KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI YA MTAA.*

Katika kuchagua viongozi wa ngazi ya Serikali ya Mtaa, tafuteni Watanzania wenye sifa zifuatazo:

(i) *Awe mchapakazi* mwenye kujitoa sadaka kuwatumikia watu, hasa wananchi wa kawaida;

(ii) *Awe mwepesi* kuona, kusikiliza na kuguswa na shida za wananchi wake. Tena awe jasiri katika kupigania haki za wanyonge na awe na uwezo na ubunifu katika kutatua kero za wananchi hao;

(iii) *Awe mwadilifu*, anayechukia na kupiga vita rushwa na ufisadi kwa matendo;

(iv) *Anayetambua fursa* zilizopo katika eneo lake, kubuni mikakati ya kuwaendeleza wananchi anaowaongoza na kuwatia watu wake hamasa ya kuthubutu kutumia fursa hizo;

(v) *Awe mtetezi hodari* wa kulinda mazingira na mpambanaji dhidi ya athari za mabadiliko ya tabianchi; 

(vi) *Mwenye kutoabudu nyadhifa*; anayetambua kuwa nafasi na vyeo tulivyopewa ni vya muda tu. Ni vya kupita! Thamani halisi ya kiongozi ni kufanya kazi kwa bidii na kuacha kumbukumbu nzuri kwa ustawi wa eneo analoliongoza na Taifa kwa ujumla; 

(vii) *Awe kama mchezaji mzuri* wa kiungo katika timu ya ushindi, anayetambua kwamba mkono mmoja hauwezi kupiga makofi ya shangwe;

(viii) *Awe mwenye kutambua kwamba kazi za kiongozi* zina maana sana kwa kuwa zinamwezesha kubadilisha maisha ya maelfu ya Watanzania, hasa wanyonge, kuwa bora zaidi;

(ix) *Awe na uwezo wa kuwaeleza wananchi kinaganaga* kuhusu Serikali yao inawapeleka wapi na wajibu wa kila mmoja ili waendelee kuiunga mkono; na

(x) *Awe anatoka ndani ya chama cha siasa(CCM)* kinachotetea maslahi na haki za wanyonge na chama hicho ni CCM!

Jumatatu, 24 Juni 2019

Mfahamu mnyama simba kiundani zaidi*

*Mfahamu mnyama simba kiundani zaidi*

Simba ni miongoni mwa wanyama ambao ni jamii ya paka, ukiondolea mbali kwamba ndiye mnyama mkubwa anayewinda katika jamii yao hiyo, lakini pia ni wanyama ambao hupenda kuishi katika makundi makundi, kwa lugha nyingine naweza sema wanaishi kifamilia kama ilivyo kwa binadamu, na familia zao huweza kuwa na simba takribani kumi na watano.

Njia rahisi ya kuwatambua kwa jinsia zao ni muonekano pamoja na majukumu, wakati simba dume shingoni likiwa limejaa manyoya Mengi, simba jike huwa na manyoya sawa mwili mzima, hapo ni kwa mtizamo wa namna wanavyoonekana.

Katika majukumu Simba hugawana, kazi ya kuhakikisha chakula cha kutosha kinapatikana katika familia hilo ni jukumu la simba jike, na simba jike aendapo mawindoni Jukumu lA simba dume ni kulinda mipaka tuu, uzito wa mnyama huyu huwa kati ya kilo 120 mpaka 240 inategemea na umri pamoja na afya.

Uhai wa simba kuishi ni kati ya miaka 10 mpaka 14 lakini kwa simba wa Africa hufika hadi miaka 17, Simba huanza kufundisha mbinu za uwindaji watoto wake tangu wakiwa wadogo kabisaa, ambapo huwatanguliza mbele na kuanza kuwabughuzi kwa kuwapiga piga ngwala, jambo ambalo hufanya watoto wake kuwa wenye hasira na wakali sana, na mbinu hizo ndio hutumia akiwa anawinda ukubwani.

Simba Mara zote hupendelea kukaa sehemu ambazo kuna miamba mizuri, pamoja na nyasi kavu kavu ambazo hufanana kwa mbali na rangi yake, kwakuwa huishi kifamilia dume ndio huanzisha makazi mapyaa, ambapo likiunguruma kwa sauti yake, sauti hiyo husafiri umbali mrefu sana na sehemu inayoishia ndio huwa mpaka wa makazi yao, na kama katikati ya sauti hiyo itakumbana na makazi ya simba wengine, basi dume jingine litaitikia, hapo kinachofuata ni simba hao kuhama lakini kama hawatakubaliana kutoka basi madume ya panda hizo mbili yatakutana kuoneshana ubabe na litakalokubali kushindwa litaondoka na familia yake.

Simba dume huchukia sana jike akizaa dume, hasira yake huja pindi anapoyafikiria madaraka, kwani hutambua jamaa hao ndio watakao kuja kumpindua ili wao ndio wawe watawala, hivyo chuki yake hukuwa kila watoto hao wanapozidi kuongezeka kimo, jukumu kubwa la kuyalinda madume hayo huwa chini ya mama yao, siku akizembea tuu Simba dume huvinyonga kikatili sana, mtifuano huo huwa hauishii kwa watoto tuu, hata Simba dume linapozeeka na kushindwa kutimiza majukumu yake kwa ustadi hufukuzwa kabisa na wanafamilia wenza na nafasi yake itachukuliwa na Simba dume ambaye anachipukia kwa wakati huo.

*Zifuatazo ndizo mbinu anazotumia simba kuwinda;*

1. Naweza sema ni mnyama pekee anayewinda kwa kutumia akili sana.

2. Ni ngumu kumuona awapo katika mawindo hasa hasa kiumbe anayewindwa.

3. Hana papara anapowinda na hutumia mahesabu makali, kwanza hutambua udhaifu wa anayemuwinda na baada ya hapo shughuri yake huanza, kama mnyama anayemuhitaji anauwezo mkubwa wa kunusa basi atacheza na upepo , kama anayemuwinda ana uwezo wa kuona mbali basi atajificha kwa ustadi sana.

4. Anayepanga kumkamata huangaika naye huyo huyo, hata kama kuna chansi ya kumkamata mwingine, simba hana tamaa na hii ni kwa sababu huofia kuharibu mahesabu ya washirika alionao katika mawindo.

5. Ni mkatili sana kwani kabla ya kumkamata windo lake cha kwanza anachokifanya ni kukiharibu kisaikolojia, ukishapaniki tuu ndio anakushughulikia.

6. Akiruka juu anapotua huongezeka uzito mara dufu, hufikia karibu kilo 300 sawa na mifuko 6 ya cement utupiwe kwa pamoja.

7. Tofauti na anapowawinda wanyama wengine akikuona mwanadamu huja kwa spidi huku mgongo wake akiupindisha kushuka chini, siku ikikutokea hali hiyo kumbuka hata kumtaja Mungu.

*Sifa zingine za mnyama huyu.*
1. Anapowinda unyayo wake huwa haugusi kabisa chini.

2. Simba ni mnyama mvivu pasina mfano, hutumia muda wake mwingi kupumzika hata kama hajachoka, takribani masaa 15 hadi 20 katika Masaa 24 hutumia kubadilisha mapozi tuu.

3. Pamoja na ukali wake wote lakini cha ajabu mnyama fisi ana uwezo wa kumnyang'anya chakula alichowinda.

4. Anapokula hapendi kabisa kelele na zikitokea kelele au harufu ambayo itamkera yupo tayali kuacha nyama aende zake.

5. Hali nyama ambayo hajawinda mwenyewe.

6. Ni mnyama ambaye anajiamini sana na anajiua kwamba anaogopwa sana.

7. Ni mnyama ambaye ana uwezo mkubwa wa kuona mbali, ikiwa ni pamoja na kusikia, uwezo wake humsaidia kuwinda wakati wowote ule anaojisikia iwe usiku au mchana.

Chakula apendacho samba.
Simba ni mnyama anayekula nyama tu, ule msemo wa kusema akikosa nyama anakula majani, hata fisi hafai kusingiziwa, simba ukiona anakula majani basi ni kwa sababu ana maumivu ya tumbo, chakula chake kikuu ni nyama na wanyama anaowapendelea sana ni pamoja na:
1. Nyati
2. Pundamilia
3. Nyumbu.
4. Mbuni
Nk.

*Pamoja kwamba Simba hujipatia kitoweo chake kwa urahisi sana, lakini baadhi ya wanyama humpa tabu sana nao ni kama wafuatao*.

1. Nyati kuna wakati wakichachamaa huweza hata kumuua simba asipowaingia kwa akili mkubwa.

2. Pundamilia hutumia vyema miguu yake ya nyuma kwa kukimbia pia kama silaha, simba wengi hupata majeraha sababu ya wanyama hawa.

3. Tembo pamoja kwamba wao ni hatari, lakini kushindwa kuwaangusha hata tembo wadogo tena wao wakiwa zaidi ya watano.